LEO NI MAADHIMISHO SIKU YA MAULIDI

Na.Issack Gerald
Waisilamu wilayani Mpanda na Mkoa wa Katavi kwa ujumla wameombwa kuhudhuria maulidi ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa Mtume Mohamadi yanayofanyika leo.
Wito huo umetolewa na Shehe wa baraza kuu la waisilamu Tanzania BAKWATA Wilaya ya Mpanda  Iddi Shabani Kondo Wakati akizungumza na Mpanda Redio ambapo amewaomba waisilamu wote kudumisha amani kataika hadhara hiyo .
Shehe Kondo amesema kuwa Maulidi hiyo itafanyika katika kata ya Stalike halmashauri ya nsimbo kuanzia saa 1:30 jioni.
Amesema katika kuadhimisha siku hiyo waisilamu wote wanakumbuka kazi iliyofanywa na mtume Mohamadi ya kufikisha ujumbe rasmi wa mafundisho wa uisilamu.
Maulidi hii ya mwaka 1439 wa dini ya kiisilamu sawa na mwaka 2017 kitaifa yatasomwa wilayani Ruangwa Mkoani Lindi na tarehe 1/12 itakuwa ndio siku ya mapumziko.

Habari Zaidi NA P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA