JAMII MKOANI KATAVI IMETAKIWA KUSHIRIKI KUWAFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU WALIOFICHWA MAJUMBANI ILI WAPATE HAKI YAO YA ELIMU

Na.Issack Gerald-Katavi
JAMII Mkoani Katavi imeaswa kushirikiana ipasavyo na kamati ya kulea baraza la watoto wenye ulemavu iliyopo Wilayani Mpanda Mkoani Katavi kwa kuwafichua watoto waliofichwa majumbani ili wapatiwe haki ya elimu.
Wanafunzi wenye ulemavu na wasio na ulemavui katika shule ya msingi Azimio Manispaa ya Mpanda wakiwa katika picha ya pamoja(PICHA NA.Issack Gerald)
Aliyevaa koti kutoka kushoto ni mratibu wa Mradi wa elimu Jumuishi Mkoani Katavi,wa pili Issack Gerald mwandishi Mpanda Radio fm pia mjumbe na katibu wa kamati hiyo,waliobaki ni baadhi ya watoto wenye ulemavu(PICHA NA.Issack Gerald)

Wito huo umetolewa leo na Meneja wa Mradi wa elimu jumuishi Tanzania Alani Kamunde wa shirika la International Aid Services,kupitia kikao cha kupokea,kujadili,kutathimini na kupanga mikakati ya namna ya kuyapatia ufumbuzi matatizo yanayowakbili watoto wenye ulemavu Mkoani Katavi.
Kwa upande wake mratibu wa mradi wa elimu Jumuishi mikoa ya Rukwa na Katavi Bi.Veronica Mavanza amesema,matatizo yanayowakabili watoto wenye ulemavu yaliyobainishwa na kamati ya kulea  baraza la watoto wenye ulemavu wameyachukua na watashirikisha jamii ipasavyo kuyapatia ufumbuzi.
Naye mwenyekiti wa kamati ya kulea baraza la watoto wenye ulemavu wilayani Mpanda Bw.Joshua Sankara ambaye pia anatoka idara ya maendeleo Manispaa ya Mpanda,amewapongeza viongozi wa mradi ngazi ya kitaifa kwa kufika mara kwa mara Mkoani Katavi kupokea changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto wenye ulemavu ambapo amesema kamati itaendelea kutoa ushirikiano katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo.
Nao baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo inayolea watoto wenye ulemavu wamesema uwepo wa mradi wa elimu Jumuishi Mkoani Katavi umesaidia jamii kutambua haki za watoto wenye ulemavu ikiwemo kuwapeleka shule na kuwapatia haki nyingine muhimu za kibinadamu.
Mradi wa elimu Jumuishi uliopo katika mikoa ya Rukwa na Katavi pekee hapa nchini ulianza mwaka 2012 na unaratibiwa na shirika la IFI lenye makao makuu Mkoani Arusha likijumuisha washirika watatu International Centre on Disabilities(ICD),International Aid Services(IAS) na kanisa la Free Pentecosatl Church Of Tanzania(FPCT).
Mtoa mada katika Kikao cha leo ambacho kimefanyika katika Ofisi za mradi wa elimu Jumuishi Mjini Mpanda alikuwa Bw.Verhan Bakari ambaye ni mshauri wa mradi wa elimu Jumuishi kutoka Mkoani Arusha mradi ambao umesaidia kupatikana kwa haki za watoto wengi waliokuwa wamenyimwa haki hasa suala la elimu kwa kufichwa majumbani.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA