AFISA ELIMU KATAVI:TUNATATHIMINI MATOKEO DARASA LA SABA 2017 TUJUE TULIPOJIKWAA TUCHUKUE HATUA

Na.Issack Gerald-Katavi
MKOA wa Katavi umesema wanajitathimini ili kubaini sababu zilizosababisha kushuka kiwango cha ufaulu katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba kwa mwaka 2017.

Kauli hiyo imetolewa leo na Afisa Elimu mkoani katavi  Mwl.Ernest Hinju wakati ambapo amesema wanafanya tathimini hiyo kwa kushirikisha wadau wa elimu kuzuia kutofanya vibaya katika mitihani ijayo.
Kiwango cha ufaulu wa darasa la saba kwa mwaka huu katika Mkoa wa Katavi kimeshuka tofauti na mwaka jana ambapo katika matokeo ya mwaka jana kati ya mikoa 26 ya Tanzania bara,Mkoa wa Katavi ulishika nafasi ya 2  kwa asilimia 86.80 na mwaka huu imeshuka kwa kushika nafasi ya 9 kwa asilimia 90.01.
Mwl Hinju akizungumzia matokeo ngazi ya Halmshauri,amesema ufaulu katika Manispaa ya Mpanda umeshuka kutoka asiliamia 96 hadi 60,Nsimbo kutoka asilimia 84 hadi 71,Mpimbwe ikishuka na kufikia asilimia 79%,Mpanda Vijijini ikishuka kutoka asilimia 66 hadi 83.
Hata hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kitaifa kwa mwaka 2017 imepanda hadi nafasi ya 6 kutoka nafasi ya 40 kwa mwaka 2016 ambapo Mlele ndiyo ambayo imeshika nafasi ya kwanza kimkoa.
Hata hivyo Mwl Hinju amesema wanachunguza kama kuna uzembe uliofanywa na watendaji kwa kila Halmshauri kuanzia walimu wakuu mpka maafisa elimu ili hatua zaidi zichukuliwe.
Nao baadhi ya wadau wa elimu Mkoani Katavi wamesema matokeo hayo huenda yametokana na kuwepo kwa ushirikiano kati ya wazazi na walimu katika kufuatilia maendeleo ya mtoto awapo shuleni.

Kwa miaka mitatu Mfululizo kuanzia mwaka 2014,Mkoa wa Katavi ulikuwa ukishika nafasi ya 1-3 huku Manispaa ya Mpanda ikishika nafasi ya 1 kwa kipindi hichohicho.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA