WAZEE MKOANI KATAVI WAOMBA SERIKALI IWATENGENEZEE MAZINGIRA RAFIKI KATIKA MASUALA YA MATIBABU-Septemba 29,2017



Na.Issack Gerald-Katavi
UMOJA wa wazee Mkoani Katavi kimeiomba serikali kuendelea kutengeneza mazingira yatakayomwezesha mzee kupatiwa huduma za matibabu bila usumbufu.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa chama hicho Mkoani Katavi Bw.Marius Bagaya wakati akizungumza na Mpanda Radio kuhusu kuelekea maadhimisho ya siku ya wazee duniani yatakayoadhimishwa keshokutwa.
 Aidha Bagaya amesema kutokana na Ofisi nyingi kuwa na wafanyakazi vijana,baadhi ya vijana wanashindwa kuwahudumia ipasavyo hasa katika ofisi za umma ambapo amewaomba vijana waliopo kaatika Ofisi mbalimbali kutambua kuwa kila mtu ni mzee mtarajiwa.
Kwa upande wake Makamu katibu wa Chama cha wazee Mkoani Katavi Bw.Nganyaga Mwendambali amesema pamoja na changamoto zinazowakabili wazee,serikali imepiga hatua katika masuala ya wazee ikiwa ni pamoja na wazee kuingizwa katika Wizara ya afya ambapo pia ameomba wazee wapate pensheni pamoja na kutengenezewa sheria itakayosimamia mahitaji yao.
Hata hivyo kwa upande wa baadhi ya wazee pamojana mambo mengine wanasema kwa sasa katika baadhi ya maeneo mkoani Katavi hawapangi msitari ambapo sera ya Mzee kwanza inazingatiwa wanapohitaji kupatiwa huduma.
Siku ya Jana mganga mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt.Yahya Hussein aliziagiza Halmashauri zote Mkoani Katavi kuhakikisha zinaandaa viatmbulisho kwa ajili ya wazee ili wapatiwe matibabu bila usumbufu ikiwa ni pamoja na huduma nyingine muhimu kwa wazee.
Mkoa wa katavi kwa mjibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 ulikadiriwa kuwa na wazee wapatao 500.
Maadhimisho ya siku ya wazee Duniani kwa mwaka 2017 yanatarajiwa kuadhimishwa mkoani Dodoma na kauli mbiyu inasema ‘’Kuelekea uchumi wa viwanda tuthamini michango,uzoefu na ushiriki wa wazee kwa maendeleo ya taifa’’.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA