TLB KATAVI WASUBIRI MWONGOZO ILI KUSHIRIKI SIKU YA FIMBO NYEUPE DUNIANI-Septemba 22,2017



Na.Issack Gerald-Mpanda Katavi
CHAMA cha watu wasioona Mkoani Katavi (TLB) kimesema kinasubiri mwongozo wa viongozi wa chama hicho ngazi ya Taifa ili wafahamu namna watakavyoshiriki maadhimisho ya siku ya watu wasioona duniani yanayotarajiwa kuadhimishwa mwezi ujao.

Hatua hiyo imebainishwa na mwenyekiti wa chama hicho Mkoani Katavi TLB Bw.Issack Mlela ambapo amesema wanatakiwa wapatikane wawakilishi 15 kutoka mkoani Katavi watakaowakilisha watu wasioona katika maadhimisho hayo yatakayofanyika kitaifa Mkoani Lindi ifikapo Oktoba 19 mwaka huu.
Kwa upande wake kaimu Mratibu wa mradi wa elimu Jumuishi Mkoani Katavi Bw.Stephano Masuluali amesema wanaendelea kuwahamasisha watu wenye ulemavu kujitokeza katika maadhimisho hayo.
Kwa upande wa Manispaa ya Mpanda kuna jumla ya watu wenye ulemavu wasioona 82 wakiwemo wanawake 35 ,wanaume 41 na watoto sita wanaosoma katika Shule ya Msingi Azimio.
Katika maadhimisho ya mwaka jana yaliyofanyika kitaifa Mkoani Mbeya Mkoa wa Katavi ulituma wawakilishi sita wa watu wasioona ambapo Halmashauri za Wilaya Mpanda ilituma wawakilishi 3,Nsimbo-1 na Manispaa ya Mpanda-2 huku Halmashauri za Mpimbwe na Mlele zikishindwa kupeleka wawakilishi kutokana na kile kinachotajwa kuwa ni ukosefu wa fedha za kuwawezesha.
Wakati huo huo Bw.Issack Mlela mwenyekiti wa chama cha wasioona Mkoani Katavi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Katavi SHIVYAWATA pamoja na Kaimu mratibu wa Mradi wa Elimu Jumuishi Mkoani Katavi unaosimamiwa na Shirika la IFI lenye washirika watatu FPCT,ICD na IAS Bw.Stephano Masuluali wanatoa wito kwa jamii kuhusu maadhimisho hayo hasa jamii kuchukuia kwa uzito masuala ya watu wenye ulemavu ili yashghulikiwe kwa wakati.
Kwa mjibu wa sheria namba 9 ya mwaka 2010 iliyopitishwa na bunge la Jamhuri ya Munngano wa Tanzania mwaka 2010,inaitaka serikali kuanzia ngazi za mitaa hadi taifa pamoja na jamii inayoishi na watu wenye ulemavu kuwajibika katika kuwapatia au kuwasaidia watu wenye ulemavu kupata mahitaji ya msingi wanayohitaji ikiwa ni pamoja na kutowanyanyasa kwa namna yoyote ile.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com ,au P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA