SITA WAHUKUMIWA MIAKA 20 JERA KWA JARIBIO LA KUUA,YUMO MWENYE UALBINO ALIYEKATWA MKONO-Septemba 1,2017



MAHAKAMA Kuu  ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga  imewahukumu  washtakiwa  sita   kati ya kumi kifungo cha miaka 20 jela baada  ya  kuwatia hatiani kwa makosa mawili ya kula njama ya kuua na jaribio la kumuua mtoto mwenye  ulemavu wa  ngozi ‘albino” Mwigulu Matonange (13) kwa kumkata mkono wake wa kushoto .

Hukumu hiyo ambayo imesomwa leo  mahakamanki hapo  imevuta hisia  ya wakazi wa Mji wa Sumbawanga akiwemo Mkuu wa mkoa wa Rukwa,Zelothe Steven aliyehudhuria  na kusikiliza hukumu hiyo hadi mwisho.
Akisoma hukumu hiyo Jaji wa mahakama Kuu  ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga Dk Adam Mambi  pia aliwaachia huru  washtakiwa wanne  baada  ya upande wa mashtaka  kushindwa kuthibitisha  bila kutia shaka  yoyote  makosa yao .
Waliohukumiwa  kutumikia kifungo cha miaka 20 jela  kila mmoja ni pamoja na   Weda Mashilimu “Baba Siha ,Ignas Sungura , James Paschal , Nickson Ngalimia Ibrahim Tela na  Faraja Jailos  “Mwezi mpya “.
Walioachiwa huru ni pamoja na Kulwa Mashilimu,Peter Said“Simon Msalaba”,Hamis Rashid na  James Ngalamio.
Jaji Dk.Mambi alisema washtakiwa  sita walitenda  makosa  hayo  kinyume  na  kifungu cha 215 cha  kanuni  ya  sheria ya adhabu Sura namba 16  iliyofanyiwa marekebisho 2002  na Kifungu 211 cha kanuni ya sheria ya adhabu .
“Katika  kosa la kwanza la kula njama  ya kuua  adhabu  yake  ni  kifun go cha miaka 14 jela  na kosa la pili  la  jaribio la kuua  adhabu yake  ni kifungo cha maisha  lakini  mahakama kwa kuangalia  maombi yaliyotolewa , kwamba  washtakiwa wote  ni kosa lao la kwanza  pia na aina ya makosa yenyewe inawahukumu  kutumikia  kila mmoja  kifungo cha miaka 20 jela ….” Alihukumu .
Kwa mujibu wa hati mashtaka mahakamni hapo  watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda makosa hayo Februari 15,2013  mchana  katika kijiji cha Msia kilichopo katika Bonde la Ziwa Rukwa  wilayani Sumbawanga.
Upande wa Mashtaka  ulioongozwa na Mwanasheria wa Serikali,Fadhili Mwandolo  uliwaita mashahidi 12 akiwemo mama mzazi wa mtoto  Mwigulu,kwa sasa  mtoto huyo anaishi nchini Marekani .
Aidha kwa upande wa  utetezi  uliokuwa na  mawakili Baltazar Chambi,Charles Kasuku,Peter Kamyalile  na Mathia Budodi   ulikuwa na mashahidi kumi .
Katika maombezi  hayo  mawakili hao waliiomba mahakama  iwaangalie washtakiwa hao kwa jino na moyo wa huru  kwa kuwa wamekaa  mahabusu   kwa miaka  minne na miezi minne .
Mwandishi:Petty Siame,Mhariri :Issack Gerald
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com  

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA