JESHI LA POLISI WILAYANI MPANDA LAWATAKA WANANCHI KURIPOTI MATUKIO KWA WAKATI ILI KUDHIBITI UHARIFU-Septemba 18,2017



JESHI la polisi Wilayani Mpanda Mkoani Katavi limewataka wananchi kushirikiana na jeshi hilo kuripoti kwa wakati matukio mbalimbali ya kiuharifu yanayoendelea kutokea wilayani Mpanda.

Wito huo umetolewa na kaimu mkuu wa Kituo cha Polisi Wilayani Mpanda Insepcta Stephen Kisaka ambaye pia ni Mkaguzi wa Polisi katika mkutano wa hadhara ambao umefanyika katika mtaa wa Mpadeco kata ya Makanyagio.
Aidha Inspecta Kisaka ambaye pia ni mlezi wa kata ya Makanyagio amewatoa hofu wananchi  kuwa siri za kiuharifu watakazozita zitahifadhiwa kwa kuwa jeshi la polisi kwa sasa linatunza siri ipasavyo kwa lengo la kutokomeza uharifu.
Kwa upande wake Polisi Kata Kata ya Makanyagio Inspecta Mwanaisha Lwano,wamawataka wananchi kutoa taarifa za ukatiri kwa watoto,wanawake na makundi mengine ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria.
Naye Mwenyekiti wa mtaa wa Mpadeco Bw.Benard Nkana ameagiza wenye nyumba wote katika mtaa huo kutopangisha watu au wageni katika nyumba zao bila kutoa taarifa kwa viongozi kinyume na hapo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mwenye nyumba.
Nao baadhi ya wananchi wa mtaa wa Mpadeco akiwemo Julius Kipeta wameomba vikundi vya ulinzi shirikishi vitakavyoundwa viwezshwe mipkopo kwa ajili ya shghuli za maendeo huku wengine wengine wakitaka ukaguzi wa waharifu ufanyike nyumba kwa nyumba vijana watakaobainika kujihusisha na uharifu wawajibishwe pamoja na wazazi wao kwa kushindwa kama sehemu ya waharifu.
Mkutano huo pia umehudhuriwa na aliyekuwa mstahiki meya wa Manispaa a Mpanda na diwani wa kata ya Mpanda Hotel Bw.Enock Gwambasa huku karibu watu 80 wakihudhuria mkutano huo.
Miongoni mwa uharifu ambao umekuwa ukitokea mara kwa mara katika mtaa wa Mpadeco ni pamoja na wizi wa mali za nyumbani  kama mifugo,pamoja na simu unaofanyika mara nyavu za madirisha zinapokuwa zimekatwa na vibaka hasa nyakati za usiku.
Wakati huo huo ajenda nyingine zilizojadiliwa katika mkutano huo ni ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Katavi pamoja na zoezi la usafi wa mtaa ambapo kwa upande wa vyumba vya madarasa wananchi wametakiwa kuchangia asilimia 20 ya nguvu ya wananchi kama kuchangia maendeleo ambapo ni sawa na matofali laki 2 kwa kila mtaa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa pamoja na kuendelea kuchangia Shilingi 2,000/= kwa ajili ya kuchangia gharama za uzoaji taka.
Mtaa wa Mpadeco ni miongoni mwa mitaa mitano ya Kata ya Makanyagio ambapo mitaa mingine ni Kigoma,Mwangaza, Kachoma na Makanyagio ambapo jumla yanahitajika matofali milioni moja kwa ajili ya ujenzi wa madarasa.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA