SERIKALI YA MTAA WA MPANDA HOTELI YAANZA KUCHUKUA HATUA WANAOKIUKA MASHARTI YA VIBALI VYA KUFYATUA TOFALI-Julai 26,2017

SERIKALI ya mtaa wa Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,imeanza kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wanaokiuka masharti ya vibali halali walivyopewa kwa ajili ya kufyatua matofali katika mtaa huo.

Afisa mtendaji wa Mtaa wa Mpanda Hotel na Msasani Bw.Alex Msabaha amesema kuwa miongoni mwa waliochukuliwa hatua za kisheria ni pamoja na wanaofyatua tofali ndani ya mita 60 za mto na eneo la hifadhi ya barabara.
Hivi karibuni Afisa Mazingira Manispaa ya Mpanda Bw.Saidi Mandua akizungumza na Mpanda Radio ,alisema kila Mkazi wa Manispaa ya Mpanda aliyepewa kibali halali cha kufyatua tofali katika manispaa ya Mpanda ,analazimika kuchangia asilimia saba ya tofali alizofyatua kwa ajili ya maendeleo ya Manispaa ya Mpanda.
Hata hivyo baadhi ya wadau wa mazingira wamesema vibali hivyo vya ufyatuaji tofali huenda vikachochea uharibifu wa mazingira hasa vyanzo vya maji ikiwa viongozi wa Manispaa wanaosimamia shughuli hizo hawatakuwa karibu na wanaofanya shughuli hizo za ufyatuaji tofali.

 Habarika zaidi na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA