WANAFUNZI WA MAFUNZO YA UFUNDI SHULE YA MSINGI MTAPENDA HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO WAPOKEA VIFAA VYA UFUNDI




Na.Issack Gerald-Katavi-Januari 30,2017
DARASA linaloendesha shughuli mbalimbali za ufundi katika Shule ya Msingi Mtapenda Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,limekabidhiwa vifaa mbalimbali vya ufundi vikiwemo vifaa vya ujenzi,ufundi seremara  na vyerehani vyenye thamani ya shilingi milioni 1,480,000.


Katika taarifa yake wakati wa kukabidhi vifaa hivyo katika ukumbi wa Ofisi ya Kata ya Mptapenda,afisa Mtendaji wa Kata ya Mtapenda Bw.Julius Msilombo pamoja na mambo mengine amesema kuwa fedha hiyo imetoka katika mfuko wa jimbo jimbo la Nsimbo.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mtapenda Mh.Eliezel Fyula ambaye alikuwa mgeni rasmi katika makabidhiano hayo pamoja na mambo mengine amewataka wanafunzi,walimu na waratibu wa kituo hicho cha ufundishaji kuhakikisha vifaa hivyo vinatunzwa ili vitumike kwa sasa na baadaye.
Aidha Mh.Fyula amewataka wanafunzi kutumia nafasi ya mafunzo waliyonayo itumike kama njia sahihi ya kujipatia uzoefu watakaoutumia katika shghuli zao mara baada ya kuhitimu.
Naye Mratibu elimu wa kata ya Mtapenda Mwalimu Frenk Sankala,akizungumza kwa niaba ya Afisa elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya nsimbo mara baada  kupokea vifaa hivyo, amesema mahitaji mengine ambayo yanahitajika ni pamoja na madarasa mawili ya kujifunzia pamoja na mbao za kutosha kama vifaa vya kujifunzia.
Nao baadhi ya walimu wa Shule ya Msingi Mtapenda akiwemo mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Geofrey Makundi mbali na kutoa pongezi kwa waliofanikisha zoezi la upatikanaji wa vifaa hivyo,wameomba juhudi za kutafuta vifaa vingine zaidi ili kuondokana na tatizo la kufundisha kwa nadharia.
Wakizungumza mara baadha ya kukabidhiwa vifaa hivyo,wanafunzi wa mafunzo ya ufundi mtapenda wamesema vifaa hivyo vitawaongezea ujuzi zaidi wa kujifunza kwa vitendo badala ya nadharia pekee.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA