KUHUSU SIKU YA AMANI DUNIANI,WAKAZI MKOANI KATAVI WASEMA HIKI



Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama-Katavi
BAADHI ya wakazi Mkoani Katavi,wameshauri siku ya amani duniani itumike kutafakari namna ya kudumisha amani iliyopo hapa nchini.
                                  

Wakizungumza na Mpanda Radio Fm,akiwemo Philbert John Mkazi wa kata ya Mpanda Hotel wamesema,amani itadumishwa ikiwa kila mtu kila mtanzania ataheshimu sheria za nchi na kutambua umhimu wa kuwa na amani hapa nchini.
Aidha wamesema,watanzania wanatakiwa kujifunza madhara yatokanayo na kukosekana kwa amani kutoka nchini jirani zenye machaufuko zikiwemo Kongo na Burundi ambapo miongoni mwa vyanzo vya uvunjifu wa amani ni mwenendo wa siasa.
Kwa mjibu wa umoja wa mataifa siku hii imeandaliwa kipekee na baraza la Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuhakikisha dunia inakuwa mahali salama pa kuishi,kutokomeza umaskini, kutokomeza vitendo vyote vya uvunjifu wa haki za binadamu na kukuza mahusiano yanayoleta na kujenga amani.
Kwa mwaka huu kitafa,maadhimisho hayo yamefanyika mkoani Dodoma na waandaaji wa siku hiyo ni Umoja wa Mataifa kupitia kituo chake cha habari kwa kushirikiana na asasi nyingine zisizo za kiserikali.
Siku ya amani huadhimishwa Septemba 21 kila mwaka,ambapo Kauli mbiu ya mwaka huu inasema “Tokomeza Rushwa, Dumisha Amani”.
Pata habari hii pia kupitia P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM
Kwa maoni au ushauri,tuma kupitia p5tanzania@gmail.com
Mwandishi : Issack Gerald Bathromeo Mashama
Mhariri :Issack Gerald Bathromeo Mashama

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA