MKUU WA WILAYA TANGANYIKA AONYA WATAKAOANDAMANA OPARESHENI UKUTA SEPTEMBA MOSI,ASEMA OPARESHENI UKUTA IWE NI KUJENGA MADARASA,KUTENGENEZA MADAWATI NA SHUGHULI NYINGINE ZA MAENDELEO.



Na.Issack Gerald Bathromeo-Tanganyika
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Saleh Mbwana Mhando,ametoa onyo kwa wananchi na wanachama wa vyama vya siasa watakaofanya maandamano ya Opareshen Ukuta katika Wilaya hiyo yanayotarajia kuanza Septemba mosi. 
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyiika Saleh Mhando
                                       

Mkuu wa Wilaya huyo ametoa onyo hilo wakati akitoa msimamo katika Wilaya yake ikizingatiwa kuwa ndiye mwenyekiti wa kamati ulinzi  na usalama ya Wilaya akisema kuwa anatekeleza agizo kutoka mamlaka ya ngazi za juu ambao wamezuia maandamano hayo.
Amesema,jeshi la Polisi Wilayani humo limejiandaa kuwadhibiti waandamanaji wote watakaoandamana ambapo amesisitiza kuwa wananchi watumie siku hiyo kufanya shughuli za maendeleo kama ujenzi wa madarasa,kutengeneza madawati na shughuli nyingine za maendeleo.
Jana Jeshi la Polisi limewakamata viongozi mbalimbali wa ngazi za juu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema wakiwemo mwenyekiti wa chama hicho taifa Bw.Freeman Mbowe,aliyekuwa mgombea wa Urais kupitia chama hicho mwaka 2015 chini ya Mwamvuli wa UKAWA na waziri mkuu mstaafu wa Tanzania Mh.Edward Ngoyai Lowassa na John Mnyika wakituhumiwa kufanya vikoa vya ndani vya chama hicho.
Opareshen Ukuta imepangwa kuzinduliwa nchi nzima ifikapo Septemba mosi mwaka huu huku maandamano yakitajwa kutokuwa na Ukomo.
Habarika zaidi na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA