ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 70 CHACHANGWA UANZISHWAJI BENKI YA WANANCHI KATAVI,WAZIRI MKUU PINDA APIGIA DEBE WANAWAKE KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA BENKI HIYO.


Na.Issack Gerald Bathromeo

Zaidi ya shilingi Milioni 70 zimechangwa na wadau wa maendeleo Mkoani Katavi kwa ajili ya kuanzisha BENKI YA WANANCHI MKOANI KATAVI.
Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania wa awamu ya NNE(wa kwanza kulia mwenye shati nyeupe) akiwa katika mkutano wa uanzishwaji wa benki ya wananchi Katavi(PICHA NA.Issack Gerald
 


Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania Mh.Mizengo Kayanza Peter Pinda ambaye alikuwa mgeni rasmi aliyeendesha harambee na kupata kiasi hicho cha fedha,ametoa rai kwa serikali ya Mkoa wa Katavi kutoa kipaumbele kwa wanawake Mkoani Katavi  kupatiwa fursa ya kunufaika katika benki ya wananchi inayoanzishwa.
Aidha Waziri Mkuu Pinda ametoa rai hiyo katika mkutano wa wadau wa maendeleo katika Mkoa wa Katavi ambao wamealikwa kushiriki katika uanzishwaji wa benki hiyo inayolenga kuinua uchumi wa mwenye kipato cha chini.
Katika hatua nyingine waziri Mkuu Pinda amezitaka Halmshauri zote 5 za Mkoa wa Katavi kuhakikisha wanawashirikisha wadau wa maendeleo katika Halmashauri zao ushirikishwaji unaokwenda sambamba na kuwaelimisha wananchi umuhimu wa benki hii.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mugoya ambaye alikuwa mwenyekiti wa mkutano wa leo, amesema kuwa benki hii ambayo mchakato wake ulianzishwa mwaka 2014 ukakwama,atahakikisha inakamilika katika kipindi cha uongozi wake mkoani Katavi kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo.
Kati ya kiasi hicho cha fedha,fedha taslimu iliyopatikana ni zaidi ya Shilingi milioni nne ambapo hata hivyo baada ya kumalizika kikao hiki cha awamu ya kwanza,Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Raphael Muhuga amesema kuwa wanatarajia kuita mkutano mwingine wa wadau wa maendeleo utakaoshirikisha wafanyabiashara ili kuchangia kiasi kingine kwa ajili ya kuwezeshwa kwa benki hiyo kukamilika ifikapo Aprili mwakani 2017.
 Mkutano huu pia umefanyika kwa kuwezeshwa na wataalamu mbalimbali wa masuala ya benki wakiwemo Bw.Rukwaro Senkolo ambaye ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Benki za Wananchi Tanzania na Evans Maseke ambaye ni Mshauri Mwelekezi na Mtaalamu wa mambo ya Kibenki ambao walikuwa wakitoa ufafanuzi wa kitaalamu kuhusu masuala ya kibenki Tanzania.
Nao baadhi ya wajumbe wa Mkutano pamoja na kusema kuwa benki hii itamwondolea usumbufu mwananchi anaoupata kutoka kwa taasisisi nyingine za kifedha kutokana na riba kubwa,wameomba riba iwe ndogo ili kumwinua kiuchumi.
Mkutano huu umewashirikisha wadau wa maendeleo ambao ni  pamoja na Wakuu wa wilaya wa wilaya za Mpanda,Mlele na Tanganyika,Wakurugenzi wa Halmshauri 5 za Mkoa wa Katavi,wakuu wa idara kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi pia wataalamu kutoka Halmshauri zote za Katavi.
Wadau wengine walioshirikishwa ni mameneja wa Benki zilizopo Mkoani Katavi,mameneja wa vyama vya ushirika mkoani Katavi,viongozi wa dini,viongozi wa vyama vya siasa,Meneja Chama kikuu cha Ushirika LATCU,wafanyabiashara,wabunge wote 8 wa Mkoani Katavi, na waandishi wa habari.
Mkoa wa Katavi unaanzisha  Benki ya wananchi kwa kushirikiana na Jumuiya Ya Benki za Wananchi Tanzania-Community Banks Association of Tanzania (COBAT) lengo zaidi likiwa ni kupata uelewa pamoja na utaratibu kuhusu manufaa ya kuwa na  benki ya wananchi katika Mkoa wa Katavi.
Mpaka sasa jumla ya Mikoa 8 kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara ya Tanzania imekwishaanzisha benki ukiwemo mikoa ya Kilimanjaro na Kagera.
Zaidi ya wadau wa maendeleo 400 wameshiriki katika mkutano huo.
 Mhariri:Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA