MATUKIO YA MAJANGA YA MOTO YAENDELEA KUTIKISA KATAVI



Jumla ya watu watatu kati ya saba waliopatwa na majanga ya moto wamefariki dunia katika matukio sita yaliyotokea yakihusisha majengo na vyombo vya usafiri.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Kaimu kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoani Katavi Inspekta Duma Mohamed wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake.
Amesema matukio hayo yametokea kwa kipindi cha mwezi Mei 28 hadi Juni 4 mwaka huu.
Amesema katika matukio hayo,vifo vya watu  wawili  na majeruhi watatu vilitokana na gari walilokuwa wakisafiria kuteketea kwa moto katika mlima Ikondwe.
Aidha Matukio mengine ni mtu mmoja kufariki dunia baada ya gari kutumbukia mto Kasimba na mwingine kujeruhiwa baada ya kugongwa na gari huku mtu mwingine akipata hasara ya fedha taslimu shilingi milioni moja laki moja na elfu hamsini katika soko la samaki Makanyagio pamoja baada ya chumba na sebule yake na  kuunguza karanga gunia moja,kitanda,mchele debe moja,gunia la mkaa na godoro.
Pamoja na Inspekta Mohamed kuwataka wakazi Mkoani Katavi kutoa taarifa ya majanga ya moto mapema kwa jeshi la zimamoto kabla ya athari zaidi kutokea,pia ametoa onyo kali watu kwa wanaotumia namba 114 maalumu kwa ajili ya kutotoa habari za matukio ya moto kwa kuwatania jeshi la polisi kinyume na matumizi ya nambahizo huku akisema kuwa watu wawili mpaka sasa wamefikishwa Polisi  kwa Tuhuma za matumizi mabaya ya namba hizo.
Magari yaliyohusika na ajali ni pamoja na ajali iliyotokea Juni mosi mwaka huu baada  ya kuteketea eneo la mlima Nkondwe na watu watu 2 kuopteza na majeruhi 3 ambapo gari halikuokolewa.
Ajali  nyingine iliyotokea Mei 28 mwaka huu  ilihusisha gari lenye namba za usajili T 725CNZ Toyota Spacila baada ya kutumbukia mtoni na mtu mmoja kufariki dunia.
Aidha Juni Mosi mwaka huu eneo la mpanda hotel  mwenesha pikipiki maarufu Bodaboda aligongwa na gari hali ya majeruhi ambapo mpaka sasa hali yake inaendelea vizuri katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda.
Mbali na matukio hayo pia matukio ya ajali ya moto yameripotiwa kutokea kwenye nyumba ya jengo la Tasaff tukio lililotokea Juni 4 mwaka huu na jengo lingine likiwa ni jengo la Ofsi ya TANROADS.
Hata hivyo baadhi ya vyanzo vya ajali hiyo ni wananchi kuchelewa kutoa taarifa mapema katika jeshi la zimamoto.
Hata chanagamoto kwa jeshi la Polisi wanakabiliwa na changamoto ya miundombinu duni ya barabara inayowezesha magari ya zimamoto kupita kufikia eneo la tukio.
Matukio ya majanga ya moto katika Mkoa wa Katavi yamekuwa yakitokea mara kwa mara na kusababisha athari kwa wakazi ikiwemo mali kuungua.
Mwandishi:Issack Gerald Bathromeo
Mhariri:Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA