RIPOTI KAMILI YA TUHUMA ZA MENO YA TEMBO: MCHUNGAJI KANISA LA MORAVIAN WILAYANI MLELE AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUKAMATWA NA MENO YA TEMBO YENYE ZAIDI YA SHILINGI MIL.90

MCHUNGAJI wa kanisa la Moravian wilaya ya mlele  mkoni Katavi Gonweli Siame amefikishwa mahakamani katika mahakama ya hakimu mkazi  mkoa wa katavi kwa kosa la uhujumu uchumi kwa kukutwa na meno ya tembo yenye thamani zaidi ya million 90.

Akisoma sahitaka hilo hakimu mfawidhi Tigagwa Tengwa wakili wa serikali jamila mzirai amesema mnamo 5 may mwaka hu mshitakiwa alikutwa na nyara hizokuwa na thamani ya milioni 90 zenye uzito wa kilo 20  
Mahakamna ilimtaka mshitakiwa kutokujibu lolote juu ya shitaka linalo mkabili kwa kuwa mahakama hiyo hauikuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri hilo la kufuatia shitaka lenye thamani ya zaidi ya milioni 10
Wakili ameieleza mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo haujakamilika  kesi hiyo imehairisha mpaka tarehe 23 mei mwaka huu na mshitakiwa amerudishwa mahabusu.
Wiki iliyopita jeshi la polisi lilipowakamata mchungaji na watuhumiwa wenzake,ilidaiwa kuwa majina yatawekwa hadharani na polisi mara baada ya upelelezi kukamilika.
Mwandishi: Issack Gerald Bathromeo
Mhariri:Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOSPOT.COM



Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA