DIWANI KATA YA KATUMBA WILAYANI MPANDA KIZIMBANI KWA RUSHWA YA ZAIDI YA SHILINGI MIL.1

TAASISI ya Kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU  mkoa wa Katavi imemfikisha kizimbani  diwani wa kata ya Katumba  kwa kosa la kujihususha na vitendo vya rushwa.

Akisoma shtaka hilo  mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Mpanda  Bw Chiganga Tengwa   mwendesha mashtaka wa TAKUKURU mkoa wa katavi Simon Buchwa  amemtaja shtakiwa kuwa ni Seneta Baraka (30) ambaye ni diwani wa kata ya katumba.
Inadaiwa kuwa mnamo tarehe 12 mei mwaka huu mshtakiwa aliomba rushwa kiasi cha shilingi milioni moja  kwa Charles Msukuma mkazi wa ivanga kata ya Katumba  ambayo ilihusiana na kumuondolea tuhuma katika mahakama ya mwanzo ya Katumba ambapo anatakiwa aondoke na mifugo yake katika makazi ya wakimbizi.
Na wakati huohuo mei 12 mwaka huu pia amedaiwa kuomba rushwa kiasi cha shilingi laki nne kutoka kwa huyohuyo Charles msukuma ikiwa ni ushawishi wa kumuondolea mifugo katika makazi ya hifadhi ya wakimbizi kata ya Katumba.
Kufuatia hatua hiyo mshtakiwa amekana kosa na kupelekwa lumande kwa kukosa kukidhi vigezo vya dhamana ambapo mahakama imeahirisha shtaka hilo hadi litakapotajwa tena  mei 31  mwaka huu kwa ajili ya kusikilizwa.
Hiyo siyo mara ya kwanza viongozi wa umma kufikishwa mahakamani kwa vitendo vya kuomba na kupokea rushwa ambapo kuanzia mwanzoni mwa mwaka 2016 vigogo wa serikali akiwemo mwanasheria mkuu wa Mkoa wa Katavi walifikishwa mahakamani kwa vitendo vya rushwa
Mwandishi:Mgeni Shabani
Mhariri:Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOSPOT.COM


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA