MALIASILI KATAVI WATUHUMIWA KUTEKETEZA ZAIDI YAN NYUMBA 40 NA MALI ZA RAIA ZILIZOKUWA NDANI



KAYA zaidi ya 40 zimechomwa moto  na mali zilizokuwa ndani Katika kijiji cha Misanga Kata ya Tongwe Halmashauri ya Tanganyika  na watu wanaosadikika  kuwa ni maliasiri.

Wakizungumza baadhi ya wakazi wa eneo hilo kijiji hicho wakazi hao wamesema wamesikitishwa na kitendo hicho kutokana na kukosa mahali pa kuishi ambapo wameiomba serikali kuingilia kati suala hilo.
Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw.Kwabi Mabula amesema tukio hilo limetokea akiwa hayupo kijijini hapo ambapo amesema hii ni mara ya pili kutendewa kitendo hicho katika kijiji chake.
Hata hivyo mwenyekiti huyo ameitaka serikali kufika eneo la tukio ikiwa ni pamoja na kujiridhisha na kuonesha mipaka ya kijiji hicho ili kuondoka migogoro inayojitokeza.
Kwa upande wake diwani wa kata hiyo Bw.Frank Markley Kibigazi  amesema atafuatilia suala hilo ili kupata ufumbuzi nakuwataka wananchi walioko nje ya bikoni kurudi katika vijiji vinavyotambulika.
Aidha diwani huyo ametaja maeneo ambayo serikali hairuhusu mwananchi yeyete kuishi eneo hilo ni Kamama,Mlofyesi,Ijamba,Kansombo pamoja na Mnimba.
Naye MBUNGE wa jimbo la Mpanda vijijini Mh .Moshi Suleman Kakoso amesema waziri wa mali asili na utalii  kwa kushirikiana na  wizara ya mali  asili wanatarajia kufanya ziara ya kuangalia migogoro iliyoko ndani ya wilaya ya Mpanda ili itatuliwe.
Ametoa Kauli hiyo  wakati akihojiwa na MPANDA RADIO FM Kuhusu Mpango wa Serikali wa  kutatua  migogoro ya aridhi kwa wakazi wanaoshi katika  maeneo ya hifadhi ikiwa ni pamoja na baadhi ya wananchi kuchomewa nyumba zao  Katika kijiji cha Misanga Kata ya Tongwe Katika Halmashauri ya  Tanganyika.
Aidha Mh.Kakoso ametoa wito kwa wananchi wanaoshi maeneo uhifadhi wa mktaba wa DWMA kama vile Sibwesa,kesekese,kaseganyama pamoja ya Kabage na baadhi ya maeneo mengine yenye mkataba huo serikali inaendelea na utaratibu ili wananchi wa maeneo hayo waishi kwa uhuru.
Mkoa wa Katavi ni miongoni mwa mikoa yenye migogoro mingi ya aridhi , ziara hiyo ya waziri itasaidia kuondokana na migogoro  ambayo imekuwa changamoto kubwa katika mkoa wa katavi.
Matukio ya kuchomwa nyumba za wakazi mkoani Katavi  siyo mara ya kwanza ambapo mwaka 2013 wakazi wa kijiji cha Luhafe walichomewa nyumba zao pamoja na mali zilizokuwemo.
Mwandishi:Issack Gerald Bathromeo
Mhariri: Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA