AHUKUMIWA JERA MIEZI 6 KWA KOSA LA WIZI MPANDA



Mahakama ya mwanzo mjini Mpanda imemhukumu mtu mmoja mkazi wa Nsemlwa kifungo cha miezi 6 jera au kulipa faini kiasi cha shilingi laki mbili na nusu  kwa kosa la wizi kinyume na kifungu cha sheria namba 265 sura 16 kanuni ya adhabu.

Akisoma hukumu hakimu mkazi  wa mahakama  hiyo mh, Sylivesta Makombe  amemtaja bw,Ally Mtaragulwa (23) mkazi wa Nsemulwa kuwa mnamo mei 2mwaka huu  majira ya saa 2na dakika 45 asubuhi aliiba cm mbili aina ya nokia na tekno zenye thamani ya shilingi laki tatu mali ya Sara Kaposwe mkazi wa kawajense.
Mshitakiwa alipopewa nafasi ya kujitetea ameiomba mahakama impunguzie adhabu kwani hahusiki na wizi wa sm hizo ametakiwa kurudisha  gharama za sm alizoiba .
Wakati huo kesi inayomkabili mchungaji wa kanisa la Moravian kwa tuhuma za meno ya tembo kukutwa katika ofisi ya kanisa lake jana imeendelea kusikilizwa na hatimaye kuahirishwa baada ya upande wa mashahidi wa mshtakiwa kudai kupewa nafasi ya kukusanya ushahidi zaidi.
Mwandishi : Vumilia Abel
Mhariri :Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA