TAKUKURU YATOA TAKWIMU YA KESI NA MALALAMIKO ILIYOYAPOKEA MWEZI JANUARI HADI MACHI 2016,TAMISEMI WAIBUKA KIDEDEA


Na.Issack Gerald-Katavi
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoani Katavi imesema kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Machi mwaka huu imepokea malalamiko 22  ya vitendo vya Rushwa.
                        

Takwimu hiyo imetolewa na Mkuu wa Takukuru Mkoani Katavi Bw .John Minyenya wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake.
Bw.Minyenya amesema kuwa taasisi zinazoongoza  kwa kuhusishwa na malalamiko ya vitendo vya Rushwa kwa kipindi hicho ni Tawala za mikoa na serikali za Mitaa(TAMISEMI) ambapo Halmashauri zina jumla ya malalamiko 14,Jeshi la Polisi malalamiko 4,idara ya mahakama lalamiko 1,idara ya afya 1,Sekta binafsi 1 na mashirika ya umma 1.
Aidha amesema,Takukuru Mkoani Katavi ina Jumla ya ya kesi 5 zinazoendelea mahakamani zikiwa katika hatua mbalimbali huku kesi 2 zilizofunguliwa katika kipindi cha mwezi Januari hadi Machi 2016 ambazo ni CC.12/2016 inayomhusu Bi.Catherine Isack Kipeta ambaye ni Afisa mtendaji wa mtaa wa Kawajense anayeshitakiwa kwa kuomba Rushwa ya shilingi Elfu thelathini(30,000/=) kinyume na kifungu cha 15 ya sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa Na.11/2007.
Amesema kuwa Mtendaji huyo alipokea hiyo fedha kutoka kwa mfanyabiashara ambaye alifungua biasahara siku ya jumamosi ambayo ni siku ya usafi.
Kesi nyingine ameitaja kuwa inamhusisha PC Peter Exavery Kashuta askari wa kituo kidogo cha polisi Mwese aliyepokea Rushwa ya Shilingi laki moja (100,000) kati ya laki saba (700,000)alizokuwa akihitaji ambapo alipokea rushwa hiyo ili kufuta kesi ya mwananchi mmoja aliyekuwa akituhumiwa kumjeruhi mwanaye baada ya kupiga na jiwekichwani.
Watakti huo huo Takukuru imetoa wito kwa wakazi Mkoani Katavi kujitokeza na kuunga mkono juhudi za TAKUKURU ili kuongeza mapambano dhidi ya vitendo vya Rushwa.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA