SILAHA 11 KATAVI ZASALIMISHWA WAKATI WA ZOEZI LA UHAKIKI,ZAIDI YA ASILIMIA 60 HAZIJAHAKIKIWA

Na.Issack Gerald-Katavi
Jumla ya silaha 11 kati ya 193 zinazomilikiwa kisheria Mkoani Katavi zimesalimishwa huku silaha 76 kati ya hizo 193 zikiwa zimehakikiwa kuanzia Machi 21 hadi Aprili mwaka huu.

Jeshi la Polisi limekuwa na utaratibu wa kutoa takwimu mbalimbali kulingana na matukio yanayoendelea kujitokeza.
Machi 21 mwaka huu,Jeshi la Polisi Mkoani Katavi lilitoa wito kwa wanaomiliki silaha kufika katika vituo vya polisi,Ofisi za serikali za mitaa kuhakiki au kusalimisha silaha lengo likiwa kudhibiti uharifu.
Kutokana na mikakati hiyo,Jumla ya silaha 11 kati ya 193 zinazomilikiwa kisheria Mkoani Katavi zimesalimishwa huku silaha 76 kati ya hizo 193 zikiwa zimehakikiwa kuanzia Machi 21 hadi Aprili mwaka huu.
Taarifa hiyo ya uhakiki imetoleewa Aprili 15,2016 na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi SSP Damas Nyanda wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini Kwake,kuhusu zoezi la uhakiki na usalimishaji  wa silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria za nchi.
Wakati huo huo zikiwa zimesalia takribani siku 32 kabla ya zoezi la uhakiki kufikia ukomo,pamoja na mambo mengine kamanda Nyanda ametoa onyo kwa watu wanaomiliki silaha ikiwa ni kutoziazimisha kwa watu wengine au makampuni na badala yake wazitumie kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.
Kwa nyakati tofauti tofauti Inspekta Jenerali wa jeshi la Polisi Tanzania IGP Ernest Mangu amekuwa akisikika akiwaagiza makamanda wa polisi mikoa yote ya Tanzania hususani Tanzania bara kusimamia zoezi la uhakiki.
Katika hatua nyingine SSP Nyanda amesema katika silaha 76 zilizohakikiwa Shot Gun ni 48 sawa na 39%,Pistol(Bastola) 16 sawa na 40%,Rifle 12 sawa na 40 huku silaha zisizohakikiwa 61% kwa Shot Gun,60% kwa Bastola,60% kwa Rifle ambapo kwa ujumla ni sawa na 39.3% kwa silaha zilizohakikiwa na 60.6% kwa silaha ambazo hazijahakikiwa.
Katika mkoa wa Katavi silaha zinazomilikiwa kihalali ni Shot Gun 123,Bastola 40,Rifle 30 wakati ikiwa hakuna gobole hata moja.
Zoezi la uhakiki na usalimishaji wa silaha linatarajia kuhitimishwa ifikapo Mei 20 mwaka huu.
Agizo la Uhakiki na usalimishaji wa silaha kwa mara ya kwanza mkoani Katavi kwa mwaka 2016 lilianza Januari 6.
Endelea kufuatilia P5 TANZANIA MEDIA, Kwa maoni au ushauri p5tanzania@gmail.com



Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA