WANAWAKE WILAYANI MPANDA WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KWA KUFANYA USAFI HOSIPTALINI


Na.Issack Gerald-Mpanda
WANAWAKE Mkoani Katavi,wameungana na wanawake wengine duniani kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

Katika Wilaya ya Mpanda maadhimisho haya yamefanyika kwa kufanya usafi katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda wakiongozwa na Mbunge wa viti maalum mkoani katvi mh.Anna Lupemmbe ili kuwasidia wagonjwa ambao hawawezi kufanya usafi.
Akizungumzia siku ya Wanawake duniani,mbunge huyo amesema kuwa wanawake wamepiga hatua kubwa ya kimaendeleo kutokana na kutambua umuhimu na nafasi yao katika jamii
Kwa upande wao wanawake wamefurahishwa na maadhimisho hayo yamewawezesha kutafakari mchango wao katika kuisaidia jamii kimaendeleo
Siku ya wanawake duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo machi 8 ambapo siku hii hutumika kujadili masula yanayowahusu wanawake ikiwa ni pamoja na kujadili namna ya kutatua changamoto zinazowakabili.
Maadhimisho haya ya mara ya 41 tangu umoja wa mataifa ulipotangaza rasmi kuanza maadhimisho haya mwaka 1975 yanaongozwa na kauli mbiyu ya ‘’50-50 ifikapo 2030,tuongeze jitihada’’.
   

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA