WANAWAKE KATAVI WASHAURIWA KUUNDA VIKUNDI ILI KUPATIWA MISAADA


Na.Meshack Ngumba-Katavi
Wanawake Mkoani Katavi wameshauriwa Kujiunga na Vikundi ili kupata fursa ya Kupewa  misaada itakayowasaidia Kujikwamua Kimaisha kwa kuanzisha Miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Ushauri huo umetolewa na Mh,Taska Mbogo Mbunge Viti maalum Mkoa wa Katavi wakati wa uzinduzi wa Vijiwe vya wanawake Katika kata za Uwanja wa ndege,Makanyagio na Nsemulwa.
Katika Uzinduzi huo Mh Mbogo ametoa Kiasi cha shilingi Milioni Moja na nusu kwa vikundi vyote ili Kusaidia Uendeshaji wa Vikundi hivyo.
Wakizungumza baada ya kupokea Msaada huo  baadhi ya akina mama waliohudhuria uzinduzi huo wamepongeza juhudi za Mbunge zinazolenga kuwatoa wanawake katika kundi la watu tegemezi katika jamii.
Mkoani Katavi kumekuwepo vikundi mbalimbali vya wanawake wanaojishughulisha na kazi mablimbali ikiwemo utengenezaji wa sabuni,ufumaji wa vitambaa huku wengine wakijishughulisha na ufugaji licha ya kuwa hakuna soko la uhakika wanakoweza kuuzia bidhaa zao.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA