RIPOTI YA PILI AJALI MTO KOGA : MIILI YA WATU WALIOKUFA MAJI MTO KOGA HADI SASA HAWAJAPATIKANA NA GARI WALILOKUWA WAKISAFIRIA.



Na.Issack Gerald-Katavi
Miili 5 ya watu waliozama katika mto Koga uliopo mpakani mwa Mkoa wa Tabora na Katavi baada ya gari walilokuwa wakisafiria kusombwa na maji tarehe Januari 26 ,2016 hawajapatikana pamoja na gari walilokuwa wakisafiria.
                                           
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dk.Ibrahim Hamis Msengi(PICHA NA Issack Gerald)

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Mkoani Katavi ambaye pia ndiye Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dk.Ibrahim Hamis Msengi wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Ofisini kwake.
Dk Msengi amesema kuwa mpaka sasa hakuna gari linaloweza kupita kutokana na maji yanayozidi kuongezeka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na maji kujaa kwa wingi.
Katika hatua nyingine Dk Msengi amesema kuwa ukarabati wa barabara ya kutoka Mpanda hadi Tabora unaendelea kufanyika kwa kiwango cha lami isipokuwa eneo lilipo daraja la mto Koga ndipo bado kuna utata kutkana na wingi wa maji hayo.
Hata hivyo katika hali ya ukiukwaji wa onyo linalotolewa na viongozi,kuna watu wanaoendelea kusombwa na maji hayo kutokana na kudharau katazo hususabi wanaotoka Tabora kuja mpanda.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA