IDARA YA ELIMU YATOA TAARIFA RASMI MFUMO MPYA WA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI KUFANYA MITHANI MWAKA 2016 MPANDA,SHULE ZISIZOSAJILIWA NJIAPANDA


Na.Issack Gerald-Mpanda
Idara ya elimu Shule za Msingi katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,imewataka wazazi na walezi wa watoto wanaosoma katika shule ambazo hazijasajiliwa mkoani katavi ikisema kuwa kuna uwezekano wa wa kupoteza pesa nyingi na wanafunzi kukosa nafasi ya kufanya mitihani mbalimbali ya shule ya msingi inayotambuliwa na Wizara ya elimu,Sayansi,Teknolojia na ufundi.

Rai hiyo imetolewa jana na Afisa elimu Taaluma Elimu ya msingi Manispaa ya Mpanda Bw.Rashid Pili katika taarifa yake ambayo ameitoa kwa vyombo vya habari.
Amesema kuwa huenda wanafunzi wengi wakakosa kufanya mtihani yao kutokana na wengi wa wanafunzi kujiunga na shule ambazo hazijasajiliwa katika Manispaa ya Mpanda na hata Mkoa wa Katavi kwa ujumla.
Aidha Bw.Pili amesema kuwa mfumo mpya wa kufanya mitihani unaoanza mwaka 2016 unahusisha wanafunzi wa darasa la pili,la nne na la saba ambapo mithani hiyo itasimamiwa na balaza la mtihani la taifa(NECTA).
Hata hivyo wazazi wameshauliwa kuwahamisha watoto wao katika shule ambazo hazijasajiliwa na kuwapeleka katika shule za serikali zilizosajiliwa au zile za binafisi.
Kwa mjibu wa taarifa hiyo,katika Manispaa ya Mpanda kuna shule 34 za serikali zitakazokuwa na vituo vya kufanyia mtihani huku shule 2 pekee zinazofundisha Kiingereza za Reimeta English Medium School na Nzera English Medium Schoolsnazo pia zikiwa zimesajiliwa wanafunzi wake kufanya mtihani.
Katika hatua nyingine,Bw.Pili amesema kuwa usajili wa wanafunzi watakaofanya mtihani ngazi ya shule ulikwishakamilika mwaka huu ambapo usajili unaoendelea kwa sasa ni kwa ngazi ya Halmashauri wakati huo huo mchakato wa kuyaingiza majina ya wanafunzi hao katika mtandao wa balaza la Mtihani NECTA ukiendelea.
Miongoni mwa shule ambazo hazijasajiliwa kwa mjibu wa Afisa elimu huyo ni pamoja na shule ya msingi Motherland ambapo mpaka sasa ina wanafunzi wanaosomea katika shule hiyo.
Usikose kitachozungumzwa na shule zenye wanafunzi zikisemekana kutsajiliwa na wanafunzi kutofanya mitihani,endelea kuwa na P5 TANZANIA MEDIA na Mpanda Radio Fm

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA