MANISPAA YA MPANDA WANG’ANGA’NIA HOSPITALI YA WILAYA YA MPANDA IWE YAO,KAKESE YAONGOZA KWA MAAMBUKIZI YA UKIMWI


Na.Issack Gerald-Mpanda
Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imesema kuwa mchakato wa kuhamisha Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kutoka katika utawala wa Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda kuwekwa katika utawala wa Manispaa unaendelea.

Hayo yamebainishwa na mganga mkuu wa Manispaa Dk.Obed Mahenge kupitia kikao cha balaza la madiwani ambacho kimefanyika jana katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda.
Kutokana na Manispaa kutokuwa na Hospitali yake ya Manispaa,Wajumbe wa kikoa wameiomba manispaa ya Mpanda mchakato wa kuhamisha hospitali katika utawal mmoja kwenda utawala mwingine ufanyike kwa haraka ili kuwaondolea adha wananchi.
Kwa upande wake afisa anayehusika na ukusanyaji wa damu salama Manispaa ya Mpanda Bi.Redgunda Mayorwa,amesem akuwa kipindi cha  mwezi Desemba mwaka jana hadi Mwezi Januari mwaka huu,amesem akuwa kiasi ch adamu kilichokusanywa ni UNIT 407.
Katika hatua nyingine ,Dk.Mahenge amesema kuwa kata ya Kakese imeendelea kupata ongezeko la watu wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ambapo kwa kipindi cha mwezi Desemba mwaka 2015 hadi Januari mwaka huu,zaidi ya watu 40 wamegundulika kuathirika.
Hata hivyo wadau mbalimbali wameshauri kuwa,kondomu,elimu ya kutosha kwa kushirikiana na wadau mbalimbali viendelee kutolewa kwa wakazi wote wa Mkoa wa Katavi.
Mkoa wa Katavi una asilimia 5.9 ya maambukizi ambapo imevuka kiwango cha asilimia kwa taifa,ambapo maambukizi asilimia ya maambukizi ni salimia 5.1.
Hata hivyo kuna uwezekano wa aslimia kuongezeka ikiwa utafiti wa vipimo vya uhakika utafanyika kwa kumekuwa na ongezeko la watu wengi kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Kuingia Mkoani Katavi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA