WAZIRI MKUU AHITIMISHA ZIARA YA SIKU MBILI KIGOMA ATAJA MKAKATI WA SERIKLAI KUPANUA BANDARI ZIWANI TANGANYIKA


Na.Issack Gerald-KIGOMA
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Halimashauri ya Manispa Kigoma Ujiji kwa kubuni miradi mbalimbali ya biashara katika ziwa Tanganyika na  tekinolojia mpya ya kukausha dagaa wanaovuliwa katika ziwa hilo.
                                              
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akikagua dagaa wanaokaushwa kitalaam kwa kutumia jua  wakati  alipozindua soko na mwaro wa kisasa wa samaki wa Kibirizi  mjini Kigom. Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Amebainisha hayo alipokuwa akizungumza na wananchi  pamoja na wafanya biashara wa kata ya kibilizi mkoani kigoma alipoanzia ziara yake mkoani humo.
Pamoja na hayo waziri mkuu amesema serikali ipo kwenye mkakati wa kupanua  bandari ya ziwa Tanganyika ili dagaa na samaki  wanaovuliwa humo waweze kupata soko na kusfiriishwa katika  nchi jilani za  Congo,Burundi na nchi nyingine
Hata hivyo waziri mkuu Kasm Majaliwa amesema kuwa atahakikisha suala la usalama unaimarishwa  kwani wavivu wa ziwa hilo walikuwa wakifanya kazi zao za uvuvi  katika mazingira sio salama.
Wakati huo huo Waziri Mkuu jana amehitimisha ziara yake ya siku mbili mchana na kurejea Jijini Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA