WASAFIRI MPANDA WALALAMIKA TRENI KUTOSAFIRISHA ABIRIA KWA MUDA MWAFAKA



Na.Issack Gerald-MPANDA
Wasafiri wa treni mkoani katavi wamelalamikia suala la kukaa muda mrefu kwenye kituo cha treni kiasi kinachowafanya kushindwa kusafiri kwa wakati unaotakiwa.

Malalamiko hayo yametolewa leo na wasafiri wanaotoka  wilayani mpanda kuelekea mkoani tabora kuwa wamekuwa wakiondoka kwa treni muda tofauti na ratiba ilivyopangwa lakini pia kutumia muda mwingi wawapo safarini.
Wasafiri hao wamekiomba kitengo husika kushughulikia changamoto zinazo wakabili ili kuondoa usumbufu unaojitokeza.
Kwa upande msimamizi wa kituo cha mpanda bwana Khatibu Nahoda amesema tatizo kubwa linalosababisha changamoto hizo ni uchakavu wa mabehewa,uchakavu wa reli pamoja na uchache wa mabehewa hivyo amewataka wasafiri kuwa na uvumilivu wakati masuala hayo yanashughulikiwa.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA