WALEMAVU KATAVI WAOMBA MITAJI NA MIRADI YA MAENDELEO KUONDOKANA NA UMASKINI



Na.Issack Gerald-MPANDA
Watu wenye ulemavu mbalimbali Mkoani Katavi wameiomba serikali ya Tanzania kuwapatia miradi ya maendeleo  pamoja na kujenga miundombinu rafiki kwao itakayowasaidia kupunguza ugumu  wa maisha.

Hayo yamebainishwa na walemavu hao wakati wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA kuhusu maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu duniani.
Baadhi ya walemavu hao ambao wamezungumza na P5 TANZANIA MEDIA ni pamoja na Katibu wa chama cha walemavu Mkoani Katavi Godfery Sadala na Kalolo Mses ambao ni waleamavu wa viungo.
Wameuomba uongozi wa Mkoa wa Katavi, kuweka Ofisi itakayokuwa chini ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda ili walemavu wapate nafasi ya kuonana na Mkurugenzi na kueleza shida zao.
Maadhimisho ya siku ya Walemavu kitaifa yamefanyika leo Mkoani Mwanza.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA