WANANCHI KATAVI WAPONGEZWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI


Na.Issack Gerald-MPANDA
Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi Dhahiri Kidavashari,ametoa pongezi kwa wananchi Mkoani Katavi,kwa kuendelea kudumisha amani katika msimu wa sikukuu za  Maulid na Krismasi.
                                            
Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi-Dhahiri Kidavashari

Kamanda kidavashari ametoa salaamu hizo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na hali ya usalama wakati wa sikukuu hizo.
Amesema kuwa,wananchi Mkoani Katavi wanatakiwa kusherehekea kwa kudumisha amani katika kuuaga mwaka 2015 na kuukaribisha mwaka mpya 2016.
Amesema ikiwa kila mwananchi atazingatia mwongozo wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977,mkoa wa Katavi utaendelea kuwa salaama wakati wote wa msimu wa sikukuu za mwaka mpya na baada ya sikukuu hizo.
Hata hivyo Kamanda,ametoa rai kwa wakazi wote Mkoani Katavi,kuripoti katika jeshi la polisi mapema dalili zinazoashiria matukio ya uharifu ili yadhibitiwe mapema kabla ya kutokea na kusababisha madhara.

Asante kwa kuendelea kunifuatilia katika mtandao huu habari za Katavi na Kwingineko habarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA