ANASWA NA NYARA ZA SERIKALI 38 KATAVI BAADHI NI PUA YA NGURUWE PORI NA KINYESI CHA FISI KWA UNDANI ZAIDI HAPA HAPAP5 TANZANIA


Na.Issack Gerald-MPANDA
Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Vitusi Chomba(36) mkazi wa Kijiji cha Senkwa Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi
amekamatwa akiwa na nyara mbalimbali za serikali ikiwemo pua ya nguruwe pori.
                                     
Kamanda wa polisi Katavi-Dhahiri Kidavashari

Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi Dhahiri Kidavashari amesema tukio hilo limetokea Mnamo tarehe 27/12/2015 majira ya saa 18:30 katika Kijiji cha Senkwa Tarafa ya Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi kwa ushirikiano na raia wema ambao walitoa taarifa kuhusu vitendo vya mtuhumiwa kujihusisha na uharibifu wa rasilimali za Taifa.
Kamanda Kidavashari ametaja baadhi ya nyara ambazo amekamatwa nazo mtuhumiwa kuwa ni pamoja na Vipande 38 vya ngozi ya samba, Vipande viwili vya ngozi ya panyapori,  Mfupa mmoja wa pundamlia, Gamba mmoja la kakakuona, Mfupa mmoja wa sungura pori, Pua ya nguruwe pori, Kwato mmoja ya mnyama aina ya muhanga, Mkia mmoja wa sungura, Kipande cha ini cha mnyama aina ya Insha na kinyesi cha fisi.
Mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi kwa hatua za upelelezi na anatarajia kufikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Hata hivyo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi anatoa wito kwa wananchi wanaojihusisha kufanya biashara haramu za magendo kama vile uharibifu wa rasilimali za Taifa mfano vitendo vya ujangili na uwindaji haramu kuacha mara moja na wajikite katika kufanya shughuli halali katika kujipatia kipato vinginevyo hatua kali za kisheria ziaendelea kuchukuliwa dhidi yao. 
Asante kwa kuendelea kunifuatilia katika mtandao huu habari za Katavi na Kwingineko habarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA