MEYA MANISPAA YA MPANDA AOMBA HOSPITALI YA WILAYA YA MPANDA KUHARAKISHWA KUWA MALI YA MANISPAA


Na.Meshack Ngumba-MPANDA
SERIKALI imeombwa Kuharakisha Mchakato wa Kuibadilisha hospitali ya Wilaya Kuwa hospitali ya halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ili Kusogeza huduma za afya kwa wakazi wa Manispaa hiyo.
                                                         
Baadhi ya majengo Hospitali ya Wilaya Mpanda

Ombi hilo limetolewa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda ambaye pia ni diwani wa Kata ya Majengo Mh,William Philip Mbogo Katika Mahojiano maalum na Mpanda Radio na P5 TANZANIA MEDIA
Katika hatua nyingine Mh Mbogo ameahidi Kushirikiana na Madiwani wa Kata zote za Manispaa ya Mpanda Kutatua Kero za wananchi ikiwemo Kusimamia Miradi ya Maendeleo inayoanzishwa Kwa Maslahi ya wananchi.
Mh,Mbogo anakuwa Meya wa Kwanza wa Manispaa ya Mpanda Kihistoria tangu halmashauri ya Mpanda ilipopandishwa daraja Kutoka halmashauri ya Mji mwezi July mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA