DAWA ZA MAGONJWA YASIYOKUWA YANAPEWA KIPAUMBELE KUANZA KUGAWIWA KESHO KATAVI


Na.Issack Gerald-MPANDA.
JAMII Mkoani Katavi imetakiwa kuzingatia utaratibu wa wataalamu wa afya juu ya matumizi ya dawa za magonjwa yasiyokuwa yanapewa kipaumbele Mkoani  hapa.

Akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Mratibu wa Magonjwa hayo Mkoani Katavi  Furahisha Chaula amesema kesho wanatarajia kuanza zoezi la ugawaji wa dawa za majonjwa ya  Ngili maji, Trakoma, Usubi ,Minyoo na Kichocho.
Amesema kuwa mtumiaji wa dawa hizo anatakiwa kula na kushiba kabla ya kutumia dawa hizo.
Aidha amesema kuwa dawa hizo ni salama, isipokuwa baadhi zinamaudhi madogo madogo yanayoweza kujitokeza ikiwemo maumivu ya kichwa,tumbo na kichefuchefu.
Zoezi hilo la ugawaji wa dawa utakaoanza kesho  Desemba Mosi linatajiwa kumalizika desemba 05 mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA