WAKAZI KATAVI WATAKA ELIMU NA KILIMO KUPEWA KIPAUMBELE NA SERIKALI YA AWAMU YA TANO


Issack Gerald-MPANDA.
ZIKIWA zimebakia siku 29 kufanyika kwa uchuguzi mkuu wa udiwani ubunge na raisi wananchi wameitaka  serikali ya awamu ya tano iboreshe  sekta ya elimu na kilimo.

Hayo yamesemwa leo na wakazi wa maeneo mbalimbali katika katika mahojiano na P5 TANZANIA ambapo imebainika kuwa changamoto hizo ni kikwazo kwa maendeleo ya taifa.
Wameongeza kuwa serikali ijayo ihakikishe inafungua masoko ya ndani na mpenyo wa masoko ya nje ili mkulima kuepuka  unyonyaji unao fanywa na wafanyabiashara wakubwa kwa kujipangia bei kwa kisingizio cha uhaba wa masoko.
Hata hivyo  wameipongeza serikali ya awamu ya nne kwa kuboresha miundo mbinu ya shule ikiwemo ujenzi wa maabara huku wakiongeza kuwa ili elimu iwe na tija serikali ya awamu ya tano itatue vikwazo vya upatikanaji wa ajira.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA