UWT KATAVI WAFANYA UTEUZI WA WAGOMBEA UBUNGE VITI MAALUMU



Na.Issack Gerald-Katavi
MKUTANO Wa umoja wa wanawake wa CCM (UWT)Mkoani Katavi  umewateua Taska Restituta Mbogo na Anna Richad Lupembe  kuwa Wagombea wa nafasi ya Ubunge Vitimaalum kwa Mkoa wa Katavi.

Akisoma Matokeo ya Uchaguzi huo Msimamizi wa Uchaguzi huo ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr Ibrahim Msengi amewataka Wanachama  wa Chama hicho Kuepuka makundi ndani ya chama na  badala yake wawaunge Mkono wanachama walioteuliwa Kuwania nafasi mbalimbali Kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Hatua ya kuteuliwa kwa wagombea hao kunakuja ikiwa ni siku chache baada ya chama cha mapinduzi CCM ngazi ya taifa kumteua John Pombe Magufuli kugombea kiti cha Urais unaotarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA