KATIBU MWENEZI CHADEMA RUKWA NA KATAVI AHAMIA CCM

NA.Issack Gerald-Katavi
Aliyekuwa Katibu mwenezi kupitia chama cha Demkrasia na Maendeleo Mikoa ya Rukwa na Katavi John Matongo ametangaza rasmi kujiondoa katika chama hicho na kujiunga na Chama cha Mpainduzi CCM.
Matongo ametangaza uamuzi huo leo katika mahoijano maalumu katika studio za  Mpanda Radio.
Amesema sababu za kijiondoa katika chama cha Chadema ni kutokana na ukiritimba na kutoshirkishwa katika vikao na mikutano ndani na nje ya chama hicho.
John Matongo ambaye pia ni Diwani wa kata ya Kashaulili anatuhumiwa na chadema kupinga baadhi ya mipango ya maendeleo ya kukijenga chama.
Katibu huyu ametumikia nafasi ya uenezi wa chama cha Chadema kwa kipindi cha miaka kumi.

Matongo anakuwa kiongozi wa pili katika ngazi ya juu wa chadema kutangaza kukihama chama cha Chadema baada ya Mbunge wa Mpanda Mjini Said Amour Arfi kutangaza kujiondoa katika chama. 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA