ASASI ZA KIRAIA ZAINGILIA KATI SUALA LA KUONDOLEWA WALIMU WA ELIMU MAALUMU SHULENI AZIMIO

Asasi za kiraia Mkoani Katavi zimelazimika kufika katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi ili kuzungumza naye kuhusu hatua ya kuwaondoa walimu waliokuwa wakifundisha watoto wenye ulemavu katika Shule ya Msingi Azimio bila kuweka wengine mbadala.

Asasi hizo zimesema katika kipindi cha mwaka 2015 mpaka sasa wanafunzi wenye ulemavu hawafundishwi masomo inavyotakiwa baada ya walimu watatu kati ya watano wa elimu maalumu waliokuwepo kuondolewa katika shule hiyo na kupangiwa majukumu mengine.
Zimesema,walimu watatu walioondolewa shuleni walipandishwa madaraja kuwa walimu wakuu katika shule zisizokuwa na watoto wenye ulemavu,mwingine akipandishwa daraja na kuwa mratibu elimu maalumu katika Manispaa ya Mpanda ambapo mpaka sasa amebaki mwalimu mmoja anayefundisha darasa la kwanza mpaka la saba.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Bw.Michael Nzyungu amesema hakuwa na taarifa ya kuondolewa kwa walimu hao na amemwagiza Afisa elimu wa Manispaa ya Mpanda kuchukua hatua za haraka ili mpaka kufikia wiki ijayo liwe limepatiwa ufumbuzi.
Shule ya Msingi Azimio yenye wanafunzi 20 wenye ulemavu kuanzia darasa la kwanza Mpaka la Saba,ina wanafunzi 3 wa darasa la saba na 3 wa darasa la nne wanaotarajia kufanya mtihani mwishoni mwa mwaka huu.
Baadhi ya asasi zilizofika katika Ofisi ya Mkurugenzi ni pamoja na Waratibu wa mradi wa elimu Jumuishi Mkoani Katavi, Shirikisho la vyama vya watu wenye Ulemavu SHIVYAWATA na wajumbe wa kamati ya kulea baraza la watoto wenye ulemavu Wilayani Mpanda.
HABARI ZAIDI NA P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA