WAKAZI WILAYANI TANGANYIKA HATARINI KUPATA KIPINDUPINDU
Baadhi ya wakazi wa
kitongoji cha Luhafwe kata ya Tongwe wilayani Tanganyika Mkoani Katavi wamesema,wako hatarini kukumbwa na magonjwa ya milipuko kuokana na maji wanayotumia kutokuwa
safi na salama.

Aidha
wamesema wanalazimika kutumia maji hayo
kwa sababu hakuna chanzo kingine kinachoweza kuwapatia maji.
Kwa
mjibu mwenyekiti wa kitongoji hicho Bw.Malaika Bujiku na katibu wake Paul
Nkingwa Mabenga wamesema mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Muhando alioneshwa
chanzo hicho lakini mpaka sasa hakuna hatua iliyochukuliwa na serikali ili
kuwanusuru wananchi na hali hiyo.
Mapema
mwaka 2016,serikali ya wilaya ya Tanganyika ilipitisha azimio la kujenga mji wa
kibiashara katika eneo la Luhafwe lakini mpaka sasa huduma za kijamii kama
shule,afya na maji bado ziko duni ambapo licha ya serikali kuahidi kuwapatia
maji safi na salama mpaka sasa hakuna utekelezaji.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED
Comments