RAIS MAGUFULI ATAKA VIONGOZI WA DINI KUJIEPUSHA NA MIGOGORO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi wa dini mbalimbali nchini kuhakikisha wanajiepusha na migogoro mbalimbali ambayo imekuwa ikiharibu sifa na heshima ya taasisi hizo za dini. 
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo wakati alipohudhuria hafla ya kumweka wakfu na kumsimika Mchungaji Jackson Sosthenes Jackson kuwa Askofu wa tano wa Kanisa la Anglikana Dayosis ya Dar es Salaam.
Kwa upande mwingine,Dkt.Magufuli amedai endapo mahali kwenye uponyaji wa mwili ukisikia kumeanza matatizo basi unapaswa kutazama jinsi taifa unaloliongoza roho zake zitakavyopotea.
Misa ya kumsimika Askofu mteule Sosthenes imefanyika leo ikiongozwa na Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania, Jacob Chimeledya.
Mbali na Rais Magufuli aliyekuwa mgeni rasmi wengine waliohudhuria ni mke wa Rais Maguli mama Janeth Mafuli,Rais mstaafu Benjamin Mkapa.
Wengine ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi,Jenerali Venance Mabeyo,Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba,Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Kamishna wa Uhamiaji,Dk Anna Makakala,na Waziri Ofisi ya Rais (Utumishi wa Umma na Utawala Bora),George Mkuchika.
Sosthenes amesimikwa kuwa askofu kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Dk.Valentino Mokiwa aliyeondolewa madarakani na uongozi wa juu wa kanisa hilo tangu mwaka jana.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA