WABUNGE WAPYA CCM WALA KIAPO BUNGENI



Mkutano wa 10 wa Bunge umeanza leo mjini Dodoma kwa wabunge wapya watatu wa CCM kula kiapo cha uaminifu mbele ya Naibu Spika,Dk Tulia Ackson.

Wakati wabunge hao wakila kiapo,takribani wabunge 50 wa upinzani walikuwa nje ya ukumbi wa chombo hicho cha kutunga sheria.
Walioapishwa ni Dk Damas Ndumbaro (Songea Mjini), Justin Monko (Singida Kaskazini)  na Dk Stephen Kisurwa wa Longido.
Pia,Dk Tulia aliomba wabunge kusimama kwa dakika moja kumkumbuka aliyekuwa mbunge wa Songea Mjini, Leonidas Gama ambaye alifariki dunia Novemba mwaka jana.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA