WANANCHI:UGAWAJI VIWANJA UPENDELEO MTUPU

Na.Issack Gerald-Katavi
Baadhi ya Wakazi wa  Mtaa wa Msasani Kata ya Mpanda Hotel  Mkoani Katavi wameendelea kushikilia msimamo wao wakutokuwa na imani na utaratibu wa ugawaji wa viwanja katika eneo la Kampuni.
Wakizunguzumza wamesema majina ambayo yametajwa kwa ajili ya kuhamia maeneo yaliyopangwa yanatoa taswira ya upendeleo.
Hata hivyo kwa upande wake Afisa mtendaji Alex Msabaha anayesimamia mitaa hiyo amesema mchakato wa  makazi mapya umefanyika na kukamilika kwa amani na kwamba muda wowote kuanzia sasa wakazi hao watapewa maeneo kwa utaratibu uliowekwa.
Mkutano huo ambao umefanyika jana ni utekelezaji wa agizo la Halmashauri ya Manispaa iliyoagiza kufanyika mkutano wa hadhara ili kuwashirikisha wananchi mchakato mzima ikiwemo majina ya wanaotakiwa kupata viwanja kama awamu ya kwanza.  
Katika Mpango huo wa ugawaji viwanja vilivyop[o mtaa wa Kampuni kata ya Misunkumilo,mtaa wa msasani utapata viwanja 75 na Mtaa wa Tambukareli viwanja 75 ambapo viwanja hivyo vimenunuliwa na mbunge kwa ajili ya wahanga wa bomoabomoa inayotarajiwa kufanyika mwezi Januari mwakani.
Zaidi ya wakazi 200 katika eneo hilo wanapaswa kuyahama makazi yao kutokana na kuwa katika hifadhi ya reli ambapo iliamuliwa kuwa wawe wameondoka ifikapo januari 2018.
 Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA