MANISPAA YA MPANDA KUCHUKUA HATUA KUSURU KUFUNGWA MACHINJIO YA NG’OMBE-Septemba 4,2017

Na.Issack Gerald Bathromeo Mashama
Jengo la machinjio ya Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda
HALAMSHAURI ya Manispaa ya Mpanda imesema inatarajia kuanza kuchimba kisima cha maji katika Machinjo yaliyopo Kata ya Mpanda Hotel kama hatua ya utatuzi wa changamoto ya uhaba wa maji mara kwa mara.

Hatua hiyo imethibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji Manispaa ya Mpanda Bw.Michael Nzyungu amebainisha hatua hiyo kufuatia Mamlaka ya Maji na usafi wa Mazingira Manispaa ya Mpansa (MUWASA) kusema kuwa haina maji ya kutosha.
Nzyungu amesema makubaliano ya uchimbaji wa kisima ili kunusuru hali ya ukosefu wa maji katika machinjio umeafikiwa leo katika vikao vya ndani vya Manispaa ambapo hatua inayofuata ni kutangaza zabuni ambapo matarajio ni kuanza kuchimbwa kisima hicho kwa takribani wiki mbili zijazo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Manispaa ya Mpanda Mhandisi Zacharia Nyanda amesema tatizo la uhaba wa maji katika machinjio ya Mpanda Hotel inatokana na kiasi kidogo cha maji kilichopo katika vyanzo.
Baadhi ya wafanyakazi wanaofanya kazi katika machinjio ya Mpanda Hotel ambao hawakutaka kutaja majina yao kwa madai kuwa wao siyo wasemaji,wamesema siku ya jana walishindwa kuchinja ng’ombe kutokana na ukosefu wa maji ambapo wamesema tatizo hilo limekuwa likitokea takribani mara nne kwa mwezi na kueleza kuwa tatizo hilo limekuwepo kwa muda mrefu.
Kwa sasa machinjio ya Mpanda Hotel yana matenki 3 ya maji yenye ujazo wa lita 12,500 ambapo kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Manispaa hata tenki la lita 2500 halijawahi kujaa maji tangu huduma ya maji ianze kutolewa katika eneo hilo la machinjio.
Ng’ombe wapatao 50 huchinjwa kila siku ambapo kila ng’ombe anayechinjwa hulipiwa shilingi 5000/=kama ushuru ambapo hata hivyo machinjio hayo yatanatarijwa kuhamishwa kutoka eneo hilo lililopo Mtaa na kata ya Mpanda Hotel baada ya kujenga machinjio makubwa nay a kisasa nje kidogo kutoka katikati ya mji.
Mwaka 2015 Mamlaka ya Chakula na dawa nchini TFDA ilifunga machinjio ya Mpanda Hotel kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchafu uliotokana na tatizo la ukosefu wa maji kwa kuwa uwepo wa uchafu ulikuwa ukihatarisha afya za walaji.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com
Barua pepe : p5tanzania@gmail.com



Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA