BABU NA MJUKU WAKE MKOANI KATAVI WALIPUKIWA NA MOTO WA NYAYA ZA KUPASULIA MIAMBA-Julai 13,2017

WATU wawili akiwemo mtoto mwenye umri wa miaka miwili na nusu wakazi wa Mtaa wa Nsemulwa Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,wamefikishwa katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda,baada ya leo kutokea mlipuko na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao.

Mganga Mkuu Hospitali ya Manispaa ya Mpanda Dk.Theopister Elisa,amewataja majeruhi ambao wamewapokea na kuwapatia matibabu katika hosiptali hiyo kuwa ni Thadeo Mandale(77) na mjukuu wake Januari Peter(2.5).
Aidha Dk.Elisa amesema Thadeo Mandale ameruhusiwa baada ya matibabu huku mjukuu wake Januari Peter akiendelea na matibabu zaidi.
Kwa upande wake kamanda wa jeshi laPolisi Mkoani Katavi ACP Damasi Nyanda,amesema mlipuko huo umesababishwa na Nyaya zinazotumika kulipua miamba ambazo zimelipuka baada ya kuunguzwa na moto wakati Thadeo Mandale akifanya usafi.
Mashuhda wa tukio hilo Bw.Mussa Nasoro na Patrick Bona,wamesema mlipuko huo umetokea majira ya asubuhi ambapo wakazi wa eneo hilo walishikwa na mshtuko wakijua kuwa ni mlipuko wa mabomu.
Habarika zaidi na p5tanzania.blogspot.com
0764491096

p5tanzania@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA