WAKULIMA CHAMA CHA MSINGI NSIMBO WATAKA WALIPWE PESA YAO



Na.Issack Gerald-Katavi-fEBRUARI 1,2017
WAKULIMA wa zao la Tumbaku wa chama cha Msingi cha Ushirika Nsimbo Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,wametaka kulipwa malipo ya mauzo ya tumbaku katika msimu wa kilimo mwaka 2015/2016.
Baadhi ya mashamba ya wakulima Nsimbo

Wakizungumza katika mkutano mkuu wa Mwaka wa chama hicho,wamesema kuwa malipo wanayodai ni madai ya awamu ya pili ambapo wanadai dola 40 kwa kila kilo iliyozalishwa katika msimu huo.
Akijibu hoja hiyo kwa niaba ya Meneja wa Kampuni ya Premium Active Tanzania inayonunua tumbaku ya wakulima wa chama hicho Bw.Iddy Ramadhani,amesema malipo yanatarajia kulipwa mwezi Februari mwaka huu ambapo amewataka wakulima kuwa wavumilivu na mara baada ya fedha kuingizwa katika akaunti ya benki husika zitalipwa kwa wakulima.
Kwa upande wake mgeni rasmi katika mkutano huo ambaye alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mwailwa Smith Pangani,pamoja na mambo mengineamewataka wakulima wa chama cha msingi ushirika Nsimbo kulima zao la kutambaku kwa kuzingatia kanuni za kilimo cha kisasa ili kulima na kupata mazao yenye ubora na kuwanufaisha.
Aidha Bw.Pangani amewataka wakulima kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda miti wakati wakiendelea na kilimo cha zao la tumbaku.
Katika hatua nyingine Bw.Pangani amewataka viongozi na bodi ya chama cha ushirika Msingi Nsimbo kuwa na maadili mema katika uongozi ili iwe mfano kwa wanaowaongoza ili kuepuka kuwakatisha tama wakulima wa chama hicho na hivyo kudhorotesha uzalishaji.
Nje ya Ukumbi Pamoja Radio imezungumza na baadhi ya wanachana ili kutoa maoni ya semina na mkutano ambao wameufanya.
Katika hatua nyingine Bw.Mahila Kiula wa Boharia ya chama cha Msingi cha Ushirika Nsimbo kimetoa taswira na mikakati ya uzalishaji tumbaku kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ambapo wamesema wanatarajia kuzalisha kilo milioni 1,250,000 huku wakitarajia wakulima 1321 kulima zao hilo.
Kabla ya mkutano wa leo,jana kulifanyika semina kwa wakulima wa chama hicho ambapo katika mkutano wa leo wakulima zaidi ya 700 kati ya zaidi ya 900 waliotakiwa kuwepo wamehudhria.
Chama cha Msingi cha Ushirika Nsimbo kinaundwa na vijiji 14 ambavyo ni Songambele ,Isanjandugu ,Mwenge, Mtakuja, Uruwila,Mtapenda,Ibindi,Isinde,Ikondamoyo,Kapalala,Matandalani,Kanoge na Mwenge Barabara

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA