HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAOMBA KUIDHINISHIWA SHILINGI BIL.24.9 MWAKA WA FEDHA 2017/2018



Na.Issack Gerald-Nsimbo Katavi
HALMASHAURI ya Wilaya ya Nsimbo Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,imeomba kuithinishiwa na serikali kuu shilingi Bilioni 24,886 ,569,000.

Kiasi hicho cha fedha kimepitishwa na baraza la madiwani katika kikao chake maalumu cha kupanga makadirio kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ili kiasi hicho kitumike kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika halmshauri hiyo iliyokusudiwa kikao ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo.
Afisa uchumi wa Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Jabir Chilumba,akisoma bajeti katika kikao hicho amesema kuwa bajeti hiyo itakapopitishwa serikalini Shilingi Bilioni 9.6 sawa na asilimia 39 zitatumika kulipa mishahara ya watumishi,Shilingi bilioni 2.1 sawa na asailimia 8% kwa matumizi ya kawaida huku shilingia bilioni 12.3 sawa na asilimia 50 zikitumika kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Katika kikao hicho maalumu cha baraza hilo ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo,aidha Bw.Chilumba amesema mapato ya ndani yanatarajia kuwa bilioni 1, 500,047,000.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mh.Raphael Kalinga pamoja na kulipongeza baraza kwa kupitisha bajeti hiyo ya mwaka wa fedha 2017/2018 amesema miradi ya maji imetengewa shilingi bilioni 4,387,999,676 ambapo kati ya kiasi hicho shilingi 4,187,999,676 zinatoka benki ya dunia na Shilingi Milioni 200 kutoka Tamisemi.
Aidha Mh.Kalinga mbali kutoa wito kwa viongozi Ngazi ya Vijiji hadi kata kutumia fedha wanazozipokea kwa malengo yaliyokusudiwa pia amesema halmashauri inategemea kipato kwa kiasi kikubwa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na migodi,minada na miara ya simu.
Wakati huo huo wakati madiwani wakisema kuwa bajeti imekidhi mahitaji ya miradi ya maendeleo katika halmshauri,kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mwailwa Smith Pangani amesema makadirio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 yamezingatia mahitaji ya wananchi.
Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikuwa imekisia kukusanya Shilingi Bilioni 1.3 ambapo hata hivyo kwa mwaka huo ilikusanya shilingi 625 ambapo kwa mwaka 2017/2018 halmashauri imekadilia kukusanya bilioni 1.5 sawa na ongezeko la asilimia 12.38 kwa mwaka 2016/2017.
Halmashauri imepanga kushughulikia vipaumbele vya maji,afya barabara na elimu katika bajeti zake.
Pata habari hii pia kupitia P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA