TFDA KATAVI YATEKETEZA TANI 2 ZA BIDHAA BANDIA ZENYE THAMANI ZAIDI YA SHILINGI MIL.6



Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini FFDA Kanda ya Magharibi Imeteketeza bidhaa mbalimbali  zisizofaa katika matumizi ya binadamu  zenye thamani ya shilingi Milioni 6 na laki 5 Ambazo ni sawa na tani 2 zilizoingizwa Kinyemela nchini.

Akiongea wakati wa Uteketezaji wa  zoezi hilo Uliofanyika katika Dampo la kutupia taka la Misunkumilo lililoko Manispaa ya Mpanda,Kaimu Meneja wa TFDA Kanda ya Mahgharibi,Dr.EDdgar Mahundi amesema bidhaa hizo ziligundulika katika Ukaguzi Uliofanyika Mwezi May mwaka huu Mkoani katavi.
Amesema kuwa baadhi ya wlivyoteketezwa ni pamoja na maziwa ya watoto yaliyokuwa hayajasajiliwa,vyakula vilivyokwisha muda wake,vipodozi na viambata vyake vilivyokwisha muda wake.
Dr.Mahundi amesema kuwa bidhaa hizo zina  madhara makubwa kwa mtumiaji pindi anapozitumia kwakuwa hazikuzingatia Ubora Unaotakiwa ambapo ametoa wito kwa wakazi Mkoani Katavi kuzingatia matumizi ya vitu vyenye ubora kwa matumizi ya binadamu.
Kwa Upande wake Mfamasia wa Manispaa ya Mpanda,Victor Kabanga amewataka wananchi kuwa makini katika kuchunguza tarehe ya kutengenezwa na kuisha kwake kwa kipindi  wanapofanya manunuzi ya bidhaa yeyote.
Aidha Dr.Herman Kimwango akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa Mpanda,amewataka wafanya biashara wote kuacha tabia ya kuuza bidhaa ambazo zinahatarisha maisha kwa watumiaji.
Hata hivyo amewataka wafanyabiashara kujiandaa kulipia vibali vya biashara zao kuanzia mwezi Julai kwaka huu kwa wale ambao vibali vyao muda utakuwa umekwisha.
 Mwandishi:Vumilia Abel
Mhariri:Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA