WIKI YA WAUGUZI MKOANI KATAVI YAZINDULIWA WAGONJWA KUPATIWA MATIBABU BILA MALIPO HADI MEI 12 KILELE CHA MAADHIMISHO


WAUGUZI na Madaktari Wilayani Mpanda Mkoani Katavi wametiwa moyo wa kufanya kazi kwa bidii na kupuuzia maneno na vitendo vya watu wanaowakatisha tamaa ya kufanya kazi za utoaji huduma ya afya kwa ufanisi.

Wito huo umetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bw.Estomihn Chang’a ambaye amemwakilisha Mwenyekiti wa Halmshauri hiyo aliyetakiwa kufungua maadhimisho hayo  ya  Wiki ya wauguzi Duniani ambapo ufunguzi huo umefanyika katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Mpanda.
Bw.Chang’a amesema ni wakati wa wauguzi na madaktari kufanya kazi bila kujali matukio na hali inayolenga kuwakwamisha katika kutoa huduma za afya kwa Wananchi.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda Dk.Naibu Mkongwa,akizungumza kwa niaba ya wauguzi na madaktari Wiaya ya Mpanda,amesema kuwa malengo yao muda wote ni kuhakikisha wanafanya kazi kwa kutoa huduma iliyo bora na kwa bidii bila kujali watu wanawakatisha tama wanapokuwa kazini.
Awali akisoma taarifa ya Maadhimisho hayo,Mwenyekiti wa chama cha Wauguzi Tanzania TANA Mkoani Katavi Dk.Augustina  Thomas,pamoja na kusema kuwa chimbuko la Maadhimisho yaliyoasisiwa na mwaasisi Dk.Florence Nightngely aliyezaliwa mwaka 1820,amesema kuwa lengo kuu la maadhimisho hayo ni kuonesha kazi nzuri za kiuuguzi na kusaidia jamii kujua elimu ya afya zao kwa ujumla.
Kwa upande wa idara mbalimbali ambazo zimewasilisha taarifa kwa mgeni rasmi zimeonesha kuwa kumekuwepo na mwitikio katika kupata vipimo na matibabu ya magonjwa yanayowasumbua.
Katika taarifa za idara hizo,idara ya afya ya uzazi na mtoto licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali wakati wa kutoa huduma ikiwemo watu kuwa na woga wa kujitokeza kupima magonjwa ya saratani yashingo ya kizazi,kwa mwaka 2016,wamefanikiwa kutoa huduma kwa watu wapatao elfu 18.
Zaidi Mratibu wa Afya ya uzazi na mtoto Wilaya ya Mpanda Dk.Gravina Kamande amebainisha.
Hata hivyo wito umetolewa kwa wakazi Mkoani Katavi kuendelea kujitokeza kuchangia damu salama ili kunusuru wagonjwa wenye uhitaji wa kuongezewa damu huku wenye matatizo ya meno nao wakitakiwa kuzingatia kanuni za afya ambapo katika takwimu ambayo imetolewa na  Mika John Mwanyama ambaye ni mkuu wa idara ya kutibu meno inaonesha kuwa kuanzia mwaka 2013 katika Wilaya ya Mpanda watu 21 wamefariki dunia kutokana na tatizo la meno kati ya hao 7 wakiwa ni wanawake ambapo kati ya hao 7 wakiwa ni wanawake wajawazito wakipoteza maisha huku walio wengi wakipoteza maisha kutokana na kuchelewa kupata huduma katika hospitali zilizothibitishwa wakipata huduma mitaani ambazo ni hatari.
Katika maadhimisho hayo,vipimo,matibabu na ushauri nasaha vinatolewa bila malipo kwa kipindi chote cha maadhimisho ya siku ya Wauguzi duniani kuanzia Mei 05 hadi 12 ambapo Mganga Mkuu Hospitali ya Wilaya ya Mpanda Dk.Naibu Mkongwa amewahakikishia wanakatavi Kuwa dawa zipo za kutosha kwa watakaofika hospitalini hapo kupatiwa matibabu bila malipo.
Kilele cha Wiki ya Mauguzi duniani  kinatarajia kufikia tamati mei 12 mwaka huu ambapo Mgeni Rasmi katika MKoa wa Katavi akitarajia kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi huku mgeni rasmi kitaifa akiwa ni Rais wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli wakati maadhimisho hayo yatakapokuwa yakifanyikia mkoani Geita.
Mwandishi : Issack Gerald Bathromeo
Mhariri :Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5 TANZANIA MEDIA

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA