BODI YA CHAMA CHA MSINGI CHA USHIRIKA MPANDA KATI YAVUNJWA



BODI ya chama cha msingi cha ushirika cha wakulima wa tumbaku maarufu kama Mpanda Kati imevunjwa.

Taarifa ya kuvunjwa kwa bodi hiyo,imesomwa na Mkaguzi watume ya maendeleo hapa nchini Bw.Eliah Richard mbele ya wanachama wa chama hicho ambapo awali aliwataka wakulima hao kuwa na utulivu.
Pamoja na mambo mengine,amesema adhabu mbali mbali zitakazochukuliwa dhidi ya viongozi waliotuhumiwa kutapanya fedha za wakulima kuwa zitatolewa kwa mujibu wa sheria za vyama vya ushirika nchini na kwamba vyombo vya sheria vitaendelea kuchukua hatua kwa wote walio patikana na hatia kufuatia uchunguzi uliofanywa na tume hiyo.
Hata hivyo,baadhi ya wakulima wamelezea kutokuridhishwa na baadhi vipengele vya hatua zilizochukuliwa kwa madai kuwa huenda usipatikane mwarobaini wa tatizo litakalotibu madai yao.
Januari 11,2016, Naibu waziri wa kilimo,mifugo na Uvuvi Mh.Tate Ole Nasha akiwa Mkoani Katavi kusikiliza kero za wakulima wa zao la tumbaku,alimwagiza mrajisi wa vyama vya ushirika hapa nchini kuunda timu ya uchunguzi na ukaguzi wa malalamiko ya wakulima waliokuwa wakilalamika fedha zao takribani milioni 600 walizodai kuwa zilikuwa zao zilizotokana na zao la tumbaku kuliwa na viongozi wa chama cha ushirika.
Wakati huo huo walidai kuwa Chama kikuu cha ushirika LATCU kimekuwa hakitetei maslahi ya wakulima wa tumbaku na badala yake kimekuwa kikiwadidimiza na kujikuta wakiendelea kuwa katika dimbwi la umaskini.
Mwandishi:Alinanuswe Edward.
Mhariri :Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuwa na P5 TANZANIA MEDIA

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA