MKUU WA WIALAYA YA MPANDA AAGIZA ARDHI YA HEKTA 45 ILIYOUZWA NA UONGOZI WA KIJIJI KINYUME CHA SHERIA KWA MWEKEZAJI KUREJESHWA KWA WANANCHI



KATIKA kutatua Migogoro ya aridhi nchini Serikali Wilayani Mpanda imeagiza kurejeshwa kwa wananchi Mara Moja kwa eneo la hekta 45 liliuzwa kinyume cha taratibu kwa mwekezaji Katika Kijiji cha Magamba.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Bw,Pazza Mwamlima Katika Mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji hicho sambamba na Kuagiza kukamatwa kwa mwenyeti wa kijiji hicho Bw,Andrea Petro Katuma ambaye hata hivyo alimaliza Muda wake.
Katika Mgogoro huo imeleezwa kuwa  Bw,Andrea Petro Katuma na wajumbe wake Katika serikali ya Kijiji waliidhinisha Kuuzwa kwa eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 45 kwa Mwekezaji anayefahamika kwa jina la Lucia Paulo Shabani Mkazi wa Mpanda Mjini  kwa Kiasi cha shilingi Milioni 9 kwa Mkataba wa Miaka 99.
Katika hatua nyingine,baadhi ya wakazi wa kata hiyo ya Magamba iliyopo manispaa ya Mpanda wameelezea kufurahishwa na hatua mbali mbali zinazochukuliwa na Serikali  katika kuwawajibisha viongozi wasio waadilifu.
Wamesema ukosefu wa maadili kwa viongozi wa umma na kufanya kazi kwa mazoea kulilitumbukiza taifa katika wimbi la umaskini.
Sanjari na hayo wakazi hao wameongeza kwa kusema kuwa zipo changamoto lukuki katika serikali za mitaa ambazo ni kikwazo kwa maendeleo, ambazo zinapaswa kutatuliwa wakitolea mfano wa migogoro ya ardhi na huduma ya afya.
Tangu Rais Dr John Pombe Magufuri aingie madarakani kumekuwa na mageuzi makubwa katika mfumo wa utawala hasa kusimamia uwajibikaji na uadilifu kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA