MAHAKAMA YA WILAYA YA MPANDA YAFUTA HATI YA MASHTAKA YA WATU WAWLI KATI YA WATATU WALIOKUWA WAKITUHUMIWA KUIBA PIKIPIKI YENYE THAMANI YA SH.MIL.1.8



MAHAKAMA ya mwanzo mjini mpanda imefuta hati ya mashta ya watu wawili kati ya watatu waliokuwa wanakabiliwa na tuhuma za wizi wa pikipiki yenye thamani ya shingi milioni moja na laki nane.

Uamuzi huo wa mahakama umekuja mara baada ya mlalamikaji kuondoa shtaka hilo na kudai ana mtambua mshtakiwa Bw Paul Willson (19)mkazi wa Nsemurwa kama mwizi wake na si mtu mwingine
Akisikiliza kesi hiyo hakimu mwandamizi David Mbembela amewataja washtakiwa ambao wameondolewa katika shtaka hilo kuwa ni Bw Jackson Willson (17) na Thadeo Nobert(19) wakiwa wote ni wakazi wa manispaa ya Mpanda.
 Mbembela ameagiza jeshi la polisi kuandaa hati ya mashtaka  ikiwa na mtuhumiwa mmoja na hatimaye ameahilisha shtaka hilo hadi litakapo tajwa tena april 21 mwaka huu.


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA