ZIARA ZA WABUNGE WA KATAVI ZASHIKA KASI KATAVI,MBUNGE VITI MAALUMU ACHANGIA SOLA KITUO CHA AFYA MPANDA


Na.Issack Gerald-Mpanda
Kituo cha afya cha Mwangaza kinachomilikwa na manispaa ya Mpanda mkoa wa katavi kimekuwa na changamoto mbalimbali  ikiwemo kukosekana kwa vitendea kazi na kupelekea wagonjwa kukosa humuma iliyo bora.

Hayo yamebainishwa na wajumbe wakamati ya bodi ya manispaa pamoja na wananchi waliohudhuria katika ziara ya mbunge wa viti maalumu kupitia CHADEMA Bi.Roda Kunchela katika ziara aliyoifanya kituoni hapo.
Wamesema kuwa wanahitaji umeme wa ziada ili kuondoa changamoto ya kukosekana kwa  umeme unapokuwa umekatika.
Akijibu na kutolea ufafanuzi  changamoto hizo Mh.Kunchela amesema amesikitishwa na swala hilo ambapo alijitolea amekabidhi Sola kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo.
Aidha amewaahidi kutatua changamoto ambazo zinahitaji utatuzi wa haraka  na kuwataka wafanyakazi kufanya kazi kwa wito ili kuhudumia jamii inayo wazunguka.
Kwa sasa wabunge wote wa Mkoa wa Katavi wanaendelea na ziara katika maeneo mbalimbali kusikiliza kero za wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA