WANANCHI KATAVI WAPONGEZA HOTUBA YA RAIS


Na.Issack Gerald-Katavi
BAADHI Ya wakazi Mkoani Katavi wamepongeza agizo la  Rais John Pombe Magufuli kwa wakuu wa Mikoa Kuhakikisha Kila mtanzania anafanya Kazi.
                                                 
Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi

Wakizungumza na P5 TANZANIA MEDIA baada ya Zoezi la Kuapishwa  kwa wakuu wa Mikoa 26 walioteuliwa,wakazi hao wamesema hotuba ya Rais Magufuli inalenga Kupunguza Malalamiko kwa serikali yanayotokana na watu wasiofanya kazi kwa kutegemea Misaada ya Serikali.
Katika hotuba yake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli amewataka wakuu hao wa Mikoa Kusimamia shughuli za Maendeleo kwa Kila mwananchi Kufanya Kazi badala ya Kukaa vijiweni na Kucheza Michezo ya pulu Muda ya Kazi.
Aliwataka wananchi watakokamatwa wakicheza  michezo ikiwemo pulu muda wa kazi,wakamatwe na wawekwe ndani hata kwa masaa mawili ili kuleta nidamu ya uwajibikaji.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA